Aziz Ki, Bares watwaa Tuzo Ligi Kuu mwezi April 2023

AJIRA MPYA ZA WIKI HII BONYEZA HAPA
AUDIOS MPYA ZA WIKI BONYEZA HAPA
VIDEOS MPYA ZA WIKI HII BONYEZA HAPA


Aziz Ki, Bares watwaa Tuzo Ligi Kuu mwezi April 2023

Aziz Ki, Bares watwaa Tuzo Ligi Kuu mwezi April 2023
KIUNGO mshambuliaji wa Klabu ya Young Africans, Stephane Aziz Ki ameshinda tuzo ya Mchezaji Bora wa Ligi Kuu ye Tanzania Bara (NBC Premier League 2022/2023) kwa mwezi Aprili, huku Abdallah Mohamed ‘Bares’ wa Tanzania Prisons akishinda tuzo Kocha Bora mwezi huo.
Mchezaji huyo wa Kimataifa wa Burkina Faso, ameshinda tuzo hiyo baada ya kuwashinda Mshambuliaji wa Simba, Jean Othos Baleke na kiungo wa Azam FC, Ayoub Reuben Lyanga, alioingia nao hatua ya Fainali, ambapo kwa mwezi huo Yanga iliifunga Kagera Sugar mabao 5-0 na ikapoteza kwa mabao 2-0 dhidi ya Simba.
Kikao cha Kamati ya Tuzo za TFF kilichokutana Dar es Salaam Jumamosi May 6, 2023, kilimchagua Aziz Ki, baada ya kuonesha kiwango kizuri mwezi Aprili na kutoa mchango mkubwa kwa Yanga, ikiwa ni pamoja na kufunga mabao matatu ndani ua dakika 135 alizocheza kwa michezo miwili ambayo Yanga ilicheza mwezi huo.
Kwa upande wa Mohammed aliwashinda Roberto Oliveira wa Simba na Daniel Cadena wa Azam alioingia nao hatua ya Fainali, ambapo kwa mwezi huo Prisons iliifunga Ruvu Shooting mabao 3-1 na Geita Gold mabao 3-1 na kupanda kutoka nafasi ya 14 hadi ya tisa katika msimamo wa Ligi Kuu ya NBC yenye timu 16.
Pia Kamati ya Tuzo imemchagua Meneja wa Uwanja wa Highland Estates uliopo Mbarali mkoani Mbeya, Omari Malule kuwa Meneja Bora wa Uwanja kwa mwezi Aprili, kutokana na kufanya vizuri katika menejimenti ya matukio ya michezo pamoja na masuala yanayohusu miundombinu Uwanjani.
PIA UNAWEZA KUSOMA👇
- FAHAMU kuhusu Azam Pesa pamoja na Makato yake
- Ada mpya za M-Pesa 2023/2024 | Makato mapya ya M-Pesa
- DOWNLOAD | NYIMBO ZA TENZI ZA ROHONI SWAHILI MIX
- Ada za M-Pesa Songesha 2022/2023
- FAHAMU Jinsi ya Kufungua Akaunti ya M-Koba Vodacom
- MFUMO wa maombi ya Kitambulisho cha Taifa (NIDA) Online
- JINSI ya kupata mikopo ya vijana na wanawake
- Namna ya Kujisajili na Premier Bet Ushinde Mamilioni
- RATIBA kamili NBC Premier League msimu wa 2022/2023
- DOWNLOAD NIDA number | Kitambulisho cha Taifa
- MSIMAMO Ligi Kuu Tanzania Bara 2022/2023
- WAFUNGAJI Wanaoongoza kwa Ufungaji Ligi Kuu
Nijuze TV ni App ambayo ukiwa nayo utaweza kutazama mechi za Ligi Kuu Tz Bara (NBC PREMIER LEAGUE) EPL, WORLD CUP, EPL, LALIGA, SERIA, LIGUE 1, BUNDESLIGA na Ligi nyingine nyingi.