Clatous Chama akutana na Rungu la TFF

AJIRA MPYA ZA WIKI HII BONYEZA HAPA
AUDIOS MPYA ZA WIKI BONYEZA HAPA
VIDEOS MPYA ZA WIKI HII BONYEZA HAPA


Clatous Chama akutana na Rungu la TFF
KAMATI ya Uendeshaji na Usimamizi wa Ligi ya Bodi ya Ligi Kuu Tanzania (TPLB) katika kikao chake cha Mei 19, 2023 ilipitia mwenendo na matukio mbalimbali ya Ligi na kufanya maamuzi yafuatayo;
Ligi Kuu ya NBC
- Mechi Namba 222: Simba SC 3-0 Ruvu Shooting FC
Mchezaji wa klabu ya Simba, Clatous Chama amefungiwa michezo mitatu (3) na kutozwa faini ya Sh. 500,000 (laki tano) kwa kosa la kumkanyaga kwa makusudi mchezaji wa klabu ya Ruvu Shooting, Abal Kassim Suleiman tukio ambalo lilitokea wakati wachezaji hao hawagombei mpira, jambo lililosababisha mwamuzi wa mchezo ashindwe kuona.
Adhabu hii ni kwa kuzingatia Kanuni ya 41:5(5.2) ya Ligi Kuu kuhusu Udhibiti kwa Wachezaji.
First League
- Mechi Namba FLT8-03: African Lyon 1-2 Rhino Rangers FC
Kiongozi wa klabu ya African Lyon ya mkoani Dar es Salaam, Salehe Hassan maarufu kama Mkele amefungiwa miezi sita (6) na kutozwa faini ya Sh. 500,000 (laki tano) kwa kosa la kumtolea lugha za kejeli na matusi Kamishna wa mchezo tajwa hapo juu ambaye alimwelekeza atoke nje ya chumba cha kuvalia wakati wa ukaguzi wa timu.
Kamishna wa mchezo wa hatua ya Nane Bora alifanya maamuzi hayo baada ya kuona kiongozi huyo wa African Lyon anafanya vurugu zilizoathiri zoezi la kikanuni la ukaguzi wa timu kwenye uwanja wa Azam Complex Aprili 25, 2023.
Adhabu hii ni kwa kuzingatia Kanuni ya 47:3 ya First League kuhusu Udhibiti kwa Viongozi.
Kamati ya Uendeshaji na Usimamizi wa Ligi inqzikumbusha klabu zote za Ligi Kuu ya NBC, Ligi ya Championship na First League kuhakikisha Viongozi na Wachezaji wake wanaendelea kufuata na kutekeleza masharti yote ya Kanuni za Ligi katika kipindi hiki cha michezo ya mtoano (play-offs) na michezo ya ukingoni mwa msimu wa 2022/2023 wa Ligi Kuu ya NBC.
Kamati inaamini huu ni wakati wa klabu kujikita katika maandalizi ya timu kiufundi kuelekea michezo hiyo na kujiepusha na masuala mengine yote yasiyo ya kiuanamichezo na yanayoweza kuchafua taswira ya Ligi zetu na mpira wetu kwa ujumla.
PIA UNAWEZA KUSOMA👇
- Ada/makato ya Lipa kwa M-pesa, Lipa kwa Simu
- ADA za LIPA kwa Airtel Mitandao Yote
- TETESI za Usajili NBC Premier League 2023/2024
- YANGA yashika Nafasi ya 9 Simba ya 10 Afrika 2022/2023
- FAHAMU kuhusu Azam Pesa pamoja na Makato yake
- Ada mpya za M-Pesa 2023/2024 | Makato mapya ya M-Pesa
- Ada zaAirtel Money 2022/2023 | Makato mapya ya Airtel Money
- ADA Mpya za Tigo Pesa (Tigo Pesa Tariffs 2022/2023)
- Ada/Makato ya HaloPesa Tanzania, Halopesa Tariffs 2023
- DOWNLOAD | NYIMBO ZA TENZI ZA ROHONI SWAHILI MIX
- Ada za M-Pesa Songesha 2022/2023
- FAHAMU Jinsi ya Kufungua Akaunti ya M-Koba Vodacom
- Namna ya Kujisajili na Premier Bet Ushinde Mamilioni
- RATIBA kamili NBC Premier League msimu wa 2022/2023
- DOWNLOAD NIDA number | Kitambulisho cha Taifa
- MSIMAMO Ligi Kuu Tanzania Bara 2022/2023
- WAFUNGAJI Wanaoongoza kwa Ufungaji Ligi Kuu
Nijuze TV ni App ambayo ukiwa nayo utaweza kutazama mechi za Ligi Kuu Tz Bara (NBC PREMIER LEAGUE) EPL, WORLD CUP, EPL, LALIGA, SERIA, LIGUE 1, BUNDESLIGA na Ligi nyingine nyingi.