Nijuze Habari App

Dalili za Saratani ya Tezi Dume

Filed in Makala by on 18/03/2023 0 Comments
Share This

JIUNGE NA GROUP LETU LA WHATSAPP HAPA


JIUNGE NA CHANNEL YETU YA TELEGRAM HAPA


AJIRA MPYA ZA WIKI HII BONYEZA HAPA


AUDIOS MPYA ZA WIKI BONYEZA HAPA


VIDEOS MPYA ZA WIKI HII BONYEZA HAPA

Dalili za Saratani ya Tezi Dume

Dalili za Saratani ya Tezi Dume, Madhara ya upasuaji wa tezi dume,Vyakula vinavyozuia tezi dume,Picha ya tezi dume,Dalili za tezi dume na tiba yake,Dalili za Saratani ya Tezi Dume,Tezi dume ni nini,Tiba asili ya tezi dume,Tezi dume na nguvu za kiume,Sababu ya kupata tezi dume,Madhara ya upasuaji wa tezi dume 

Dalili za Saratani ya Tezi Dume

SARATANI YA TEZI DUME

Moja ya maradhi yanayoshuhudia kampeni kubwa kukabiliana nayo katika miaka ya hivi karibuni duniani ni pamoja na saratani ya tezi dume kutokana na ukubwa wa athari inazosababisha.

Ni maradhi yanayoshika nafasi ya tatu kwa kusababisha vifo vinavyotokana na saratani kwa wanaume duniani.

Pia ni chanzo kikuu cha vifo vinavyosababishwa na saratani kwa wanaume wenye umri wa miaka 70 na kuendelea.Hata hivyo, satarani ya tezi dume kwa sasa inawapata zaidi wanaume kuanzia miaka 25.

Maana ya saratani
Saratani maana yake ni ukuaji holela bila mpangilio wa seli baada ya kuparanganyika kwa mfumo wa seli unaodhibiti ukuaji na uhai wake. Na uvimbe wa kawaida wa tezi maana yake ni kuwa seli zimetutumka tu lakini hakuna mparanganyiko wa seli wala kukua kwa kusambaa kiholela kama ilivyo kwa saratani.

Hivyo, ndio maana kuna tatizo la kuvimba tezi dume na wengine kupata saratani ya tezi dume kwa wanaume wenye umri mkubwa.

Tezi dume ni sehemu mojawapo ya mfumo wa uzazi wa kiume. Inaundwa na sehemu mbili ambazo zimeunganishwa na kufunikwa kwa nje kwa utando wa tishu.

Tezi hii ipo mbele kidogo ya puru (rectum) na chini kidogo ya kibofu cha mkojo. Tezi dume inauzunguka mrija unaounganisha kibofu cha mkojo na uume (urethra).

Kazi ya tezi dume
Mojawapo ya kazi za tezi dume ni kutoa majimaji yanayochanganyika na mbegu za kiume (sperms) wakati wa kilele cha tendo la kujamiana. Mchanganyiko huu wa mbegu pamoja na majimaji hayo hutengeneza shahawa (semen).

Majimaji hayo husaidia kuzipa mbegu za kiume nguvu ya kusafiri kwenye uke mpaka kufikia kwenye mirija ya uzazi, tayari kwa utungisho na yai la kike.

Vilevile husaidia kupunguza hali ya kitindikali iliyopo katika uke, ambayo isiporekebishwa, huua mbegu nyingi za kiume na kufanya utungisho kuwa wa tabu..

Vyanzo Vinavyopelekea Tezi Dume Kutanuka:
Tatizo la kutanuka kwa tezi dume limekuwa kwa kasi sana hii ni kutokana na mitindo ya maisha wanaume wengi wanayoishi. Pia na elimu ndogo iliyoko kwenye jamii kuhusu afya zao.

Vifuatavyo ni vyanzo vya kutanuka kwa tezi dume:
– Ukosefu wa lishe kamili na Virutubisho muhimu mwilini.
– Uwepo wa sumu nyingi mwilini.
– Kutokufanya mazoezi.
– Matumizi ya pombe kali, na uvutaji wa sigara.
– Uzito mkubwa (uliopindukia, uliokithiri), na Kitambi.
– Kutokukaa sawa kwa vichocheo vya mwili (Hormone Imbalance).
– Msongo wa mawazo (Stress).
– Magonjwa ya zinaa.
– Umri mkubwa.
– Upasuaji wa korodani, kuzaliwa na korodani moja.
– Historia ya Familia (Kurithi).
– Mazingira (Ethnicity).

Dalili za Saratani ya Tezi Dume

  • Udhaifu katika utoaji wa mkojo, mkojo hauishi.
  • Kwenda kukojoa mara kwa mara.
  •  Damu ndani ya mkojo.
  • Kushindwa kukojoa.
  • Maumivu ya kiuno na mifupa ya nyonga.
  • Wagonjwa wengi huanza maumivu ya nyonga kama ni dalili za awali.
  • Udhaifu katika utoaji wa mkojo pia kunaweza kutokea kwa kuvimba kwa tezi dume bila ya saratani.
  • Damu kwenye mkojo nakushindwa kumaliza mkojo ni ishara tosha ya kuwa  tezi dume imeathirika.

Dalili za mtu aliyeathirika

  • Maumivu ya mifupa hasa chini ya mgongo, kiuno na mbavu
  • Miguu kuwa dhaifu
  • Kushindwa kumudu tendo la ndoa, au Kuhisi maumivu makali wakati unamaliza tendo la ndoa
  • Kushindwa kuzuia mkojo, pindi unapohisi kukojoa
  • Kushindwa kuzuia haja kubwa (kinyesi cha maji maji)
  • Tumbo kuja gesi mara kwa mara

UCHUNGUZI

Wanaume wote wanapaswa kufanya uchunguzi wa saratani ya tezi dume kuanzia miaka 50. Kwa wale wenye historia katika familia wanapaswa kuanza wakiwa na umri wa miaka 45.

Uchunguzi unafanyika kwa njia zifuatazo

  • Uchunguzi kwa cancer marker kwa kuchunguza damu (PSA).
  • Uchunguzi kwa njia ya kipimo cha njia ya haja kubwa (DRE)
  • Biopsy.
  • Ultrasound.
  • X-ray.
  • Bone scan.

Jinsi ya kutibu saratani ya tezi dume

  • Upasuaji.
  • Mionzi
  • Dawa ya saratani
  • Homoni.

Matibabu hutegemea

  • Ngazi na ukali wa ugonjwa.
  • Je, ugonjwa upo ndani ya tezi dume tu au umesambaa.
  • Umri na afya ya mgonjwa.
  • Magonjwa ambatanishi na saratani hiyo, shinikizo la damu, matatizo ya moyo na kisukari.

 TIBA

 UPASUAJI

  • Kuondoa tezi dume yote peke yake inaweza ikatosha.
  • Kuondoa tezi dume na tezi jirani.
  • Kuondoa tezi dume na kuhasi
  • Kuondoa tezi dume kidogo kupitia njia ya mkojo na kumpa mgonjwa tiba shufa.

MIONZI.

  • Sawa na upasuaji inaweza kuondoa ugonjwa iwapo haujasambaa.
  • Mionzi pia hutolewa kama tiba shufaa.

DAWA YA SARATANI

 

MKWANJA Mrefu Upo Premierbet Leo, kupata odds za Kibabe Tafadhali Bofya HAPA JISAJILI, BASHIRI Utusue.

 
 

Karibu Helabet Upige MKWANJA hadi 300,000, Kujiunga Bofya HAPA, Promo Code ya Bonasi Weka NIJUZE, JISAJILI, Deposit na Utusue.

 

Baadhi ya wagonjwa hufaidika na tiba hii, dawa hutolewa kwa muda mfupi na kufuatilia maendeleo ya mgonjwa kwa kufanya PSA,dawa inaweza kuwa moja au mchanganyiko.

HOMONI

Hutolewa mfullulizo kwa njia ya vidonge au sindano.

Ufuatiliaji wa karibu

Ni muhimu kufuatilia hali ya tezi isirejee baada ya ugonjwa kutibiwa kwa kufanya kipimo cha PSA mara kwa mara angalau miezi mitatu mara moja.

Madhara ya Tezi Dume Iliyotanuka:

  • Kibofu cha mkojo kuuma: hivyo hupelekea mkojo kurudi juu, na kuharibu figo na Ini … … n.k.
  • Kufunga kwa njia ya mkojo kabisa
  • Figo kushindwa kufanya kazi (Kidney Failure)
  • Kushindwa kumudu tendo la ndoa (Ndoa zinavunjika)
  • Ugumba (Infertility, Frigidity for men)
  • Kutokea kwa majipu sehemu ya Tezi Dume
  • Kifo
Saratani ya tezi dume inatibika?
Ndiyo! Kuna njia kadhaa za matibabu ya saratani ya tezi dume. Hata hivyo uamuzi wa njia gani itumike unategemea ushauri na maoni ya daktari kulingana na hatua ya ugonjwa ulipofikia na umri wa mgonjwa husika.
Katika hatua za awali za ugonjwa, daktari anaweza kushauri mgonjwa atibiwe kwa kufanyiwa upasuaji na tiba ya mionzi, wakati kwa wagonjwa wazee, daktari anaweza kushauri kumfuatilia mgonjwa kwa ukaribu bila kumfanyia upasuaji au bila kumpatia tiba ya mionzi.
Iwapo saratani imesambaa na kuathiri sehemu nyingine za mwili, matibabu yake yanaweza kujumuisha upasuaji wa kuondoa korodani, matumizi ya dawa za kupunguza kiwango cha homoni ya testosterone katika damu (hormonal therapy), au matumizi ya kemikali za kuua seli za saratani (chemotherapy).
 
Upasuaji
Upasuaji hufanyika kwa wagonjwa walio katika hatua za awali za ugonjwa (stage I na stage II) ingawa pia hufanywa kwa baadhi ya wagonjwa walio katika hatua za mwisho za ugonjwa huu yaani stage III na stage IV. Upasuaji unaofanywa ni ule wa kuondoa tezi dume pamoja na baadhi ya tishu zinazozunguka tezi hiyo.
Tiba ya Mionzi
Hii ni aina ya tiba inayotumia mionzi kuua seli zenye saratani. Tiba ya mionzi hutumika kutibu saratani ya tezi dume ambayo haijasambaa kwenye sehemu nyingine za mwili. Aidha inaweza pia kutumika kuua masalia ya tishu zenye saratani mara baada ya kufanyika kwa upasuaji.
Kwa wagonjwa walio katika hatua ya mwisho ya saratani yaani wale ambao saratani tayari imeshasambaa mwilini, mionzi hutumika kupunguza maumivu makali ya mifupa.
Madhara anayoweza kupata mgonjwa kutokana na aina hii ya tiba ni pamoja na kushindwa kusimamisha uume au uhanithi, kukosa hamu ya kula, uchovu, ngozi kubabuka, kuharisha na kutoa mkojo uliochanganyika na damu.
Tiba ya Homoni
Hii ni aina ya tiba inayotumia dawa zinazopunguza kiwango au ufanyakazi wa homoni ya testosterone mwilini. Testosterone ni homoni ya kiume inayochochea ukuaji wa tezi dume, hivyo basi matumizi ya dawa hizi husaidia kupunguza ukuaji huu na kusambaa kwa seli za saratani.
Tiba ya homoni hutolewa kwa wanaume walio katika hatua za mwisho za ugonjwa huu kwa nia ya kupunguza maumivu na kutibu dalili za ugonjwa. Dawa zinazotumika kwa tiba ya aina hii zimegawanyika katika makundi mawili, zile zinazochagiza uzalishaji wa homoni ya luteinizing (luteinizing hormone-releasing hormones, LH-RH) kwa mfano goserelin, nafarelin na leprolide; na zile zinazozuia ufanyaji kazi wa homoni ya androgen kwa mfano flutamide, bicalutamide na nilutamide.
Madhara yanayoweza kusababishwa na utumiaji wa dawa hizi ni pamoja na kichefuchefu na kutapika, upungufu wa damu, kuongezeka uzito, uhanithi na kukosa hamu ya tendo la ngono, matatizo katika ini na matiti kuwa makubwa.
Baadhi ya madaktari hutumia upasuaji wa kuondoa korodani kama njia ya kupunguza kiwango cha homoni za kiume mwilini kwa kigezo kwamba kiwango kikubwa cha homoni hizi huzalishwa kwenye korodani. Hata hivyo tiba hii haifanyiki mara kwa mara.
Baada ya matibabu?
Baada ya matibabu, mgonjwa wa saratani ya tezi dume hufuatiliwa kwa ukaribu kuhakikisha kuwa saratani haisambai sehemu nyingine za mwili. Ufuatiliaji hujumuisha mgonjwa kufanyiwa uchunguzi wa mara kwa mara pamoja na kupima PSA kwa kipindi cha miezi mitatu mitatu mpaka mwaka mmoja.

Athari zitokanazo na matibabu mbalimbali yaliyotajwa.

Upasuaji

Unaweza kusababisha kutoweza:

  • Kuzuia mkojo
  • Kupoteza nguvu za kiume.

Homoni

  • Homoni huongeza joto mwilini
  • Kupungukiwa na nguvu za kiume

Nijuze TV ni App ambayo ukiwa nayo utaweza kutazama mechi za Ligi Kuu Tz Bara (NBC PREMIER LEAGUE) EPL, WORLD CUP, EPL, LALIGA, SERIA, LIGUE 1, BUNDESLIGA na Ligi nyingine nyingi.

Download App ya Nijuze Habari Playstore tukutumie Habari zote kwenye Simu yako BILA MALIPO BOFYA HAPA.

Share This

Tags: , , , , , , , ,

About the Author ()

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *