Fainali ya CAF kuchezwa nyumbani na Ugenini

Filed in Michezo by on 19/05/2023 0 Comments
Share This
NIJUZE HABARI WHATSAPP GROUP

AJIRA MPYA ZA WIKI HII BONYEZA HAPA


AUDIOS MPYA ZA WIKI BONYEZA HAPA


VIDEOS MPYA ZA WIKI HII BONYEZA HAPA

Nijuze TV App, Mpira Kiganjani Mwako

Fainali ya CAF kuchezwa nyumbani na Ugenini

Fainali ya CAF kuchezwa nyumbani na Ugenini, Zawadi za CAF Champions League,CAF fixtures,CAF matches today live, CAF Confederation Cup 2023, CAF Champions League 2023

Fainali ya CAF kuchezwa nyumbani na Ugenini, Zawadi za CAF Champions League,CAF fixtures,CAF matches today live, CAF Confederation Cup 2023, CAF Champions League 2023

Fainali ya CAF kuchezwa nyumbani na Ugenini

Moja kati ya vitu ambavyo mashabiki wa mchezo wa mpira wa miguu wamekuwa wakivilalamikia katika mashindano ya klabu Bingwa Afrika na Kombe la shirikisho Afrika, uamuzi wa michezo ya Fainali kuchezwa nyumbani na Ugenini kama michezo ya hatua ya Makundi au Robo Fainali na Nusu Fainali.

Majibu ya swali hili yalishajibiwa tayari na aliyekuwa Rais wa Shirikisho la Mpira Barani Africa (CAF), Ahmad Ahmad alipokuja kuzindua Mashindano ya AFCON ya chini ya umri wa miaka 17 nchini Tanzania.

Sababu Kuu ni moja tu ambayo Ahmad aliitaja kuwa ni issue ya Mashabiki , Mashabiki wetu wa Africa bado hawana Ile passion au wapo wenye passion lakini hawapo vizuri kiuchumi hivo ni ngumu Kwa Mashabiki kusafiri kwenda nchi nyingine.

Kikao cha kamati kuu ya Shirikisho la Soka barani Afrika kilichokaliwa July 03, 2022 nchini Morocco kiliadhimia mabadiliko ya uchezwaji wa mechi za Fainali za CAF Interclub (CAF Champions League na CAF Confederation Cup).

Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika CAF Ahmad Ahmad na alipokuwa nchini aliulizwa kuhusiana na utaratibu huo, kuwa hawaoni kama inapoteza mvuto? Kwa nini wasiige mfano wa michuano kama ya Ligi ya Mabingwa Ulaya ambayo imekuwa ikichezwa Fainali katika Mjini mmoja ambao huchaguliwa mapema?

Ahmad alijibu kuwa “Unajua Ulaya wameelimika sana kuhusu mpira hawaoni kuwa timu hii imetoka sehemu nyingine au imetoka sehemu gani wanaona mpira ni mpira unaowavutia lakini Afrika wanaangalia timu kwa mfano hapa Tanzania, ukileta timu kutoka nje hawatovutika Uwanjani ,wanapenda Simba au Yanga kama ukiweka mechi ya Simba au Yanga uwanja utajaa, hilo linatufanya tushindwe kufanya maamuzi kuweka Fainali ya mechi moja. Unajua sio jambo la kawaida kufuata mifano ya Ulaya”

Maadhimio yaliyofikiwa ni kwamba;

1.Fainali itakuwa mechi mbili, nyumbani na ugenini huku Bingwa akiamuliwa kwa Aggregate.

2.Kama Aggregate itakuwa sawa, basi yataangaliwa matokeo timu zilivyocheza ugenini nani alipata matokeo bora zaidi na huyo ndiye atakuwa Bingwa.

3.Na ikitokea wakalingana kila kitu, basi Bingwa atapatikana kwa mikwaju ya penati .

Aidha Maboresho haya yataanza kutumika msimu huu wa mashindano 2022|2023.

Klabu ya Yanga baada ya kutinga Fainali ya Kombe la Shirikisho Afrika Sasa itanzia nyumbani kwenye Uwanja wa Benjamin Mkapa Jijini Dar es salaam May 28 dhidi ya USM Alger na mchezo wa pili utachezwa June 03,2023 nchini Algeria.

Totals Africa Cup Of Nations,CAF | History,Total CAF Champions League,Total CAF Confederation Cup,Competitions

PIA UNAWEZA KUSOMA👇

Nijuze TV ni App ambayo ukiwa nayo utaweza kutazama mechi za Ligi Kuu Tz Bara (NBC PREMIER LEAGUE) EPL, WORLD CUP, EPL, LALIGA, SERIA, LIGUE 1, BUNDESLIGA na Ligi nyingine nyingi.

Download App ya Nijuze Habari Playstore tukutumie Habari zote kwenye Simu yako BILA MALIPO BOFYA HAPA.

Download App ya Nijuze TV Utazame mechi zote kwenye Simu yako BOFYA HAPA

Share This

Tags: , , , , , , , , , ,

About the Author ()

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *