KAMATI ya watu 14 yaundwa kutatua mgogoro wa Wafanyabiashara Kariakoo

AJIRA MPYA ZA WIKI HII BONYEZA HAPA
AUDIOS MPYA ZA WIKI BONYEZA HAPA
VIDEOS MPYA ZA WIKI HII BONYEZA HAPA


KAMATI ya watu 14 yaundwa kutatua mgogoro wa Wafanyabiashara Kariakoo

KAMATI ya watu 14 yaundwa kutatua mgogoro wa Wafanyabiashara Kariakoo
WAZIRI Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Kassim Majaliwa ameunda tume ya watu 14 ambayo itachakata kero na mapendekezo ya Wafanyabiashara wa Soko la Kimataifa la Kariakoo.
Waziri Mkuu, Majaliwa ameunda tume hiyo May 17, 2023 alipozungumza na Wafanyabiashara wa Soko hilo katika viwanja vya Mnazi Mmoja vilivyopo Jijini Dar es Salaam.
Tume hiyo ambayo imepewa siku 14 kuja na mapedekezo ya kutatua changamoto za Wafanyabiashara, itakuwa na Watendaji saba kutoka Serikalini na saba kutoka Jumuiya ya Wafanyabiashara.
Kwa upande wa Serikali, Waziri Mkuu amewataja Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera Bunge na Uratibu), Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango, Katibu Mkuu
Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Katibu Mkuu Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto, Katibu Tawala Mkoa wa Dar es Salaam, Kamishna wa Kodi za Ndani wa TRA, Kamishna wa Sera wa TRA.
Kwa Upande wa Wafanyabiashara ni Mwenyekiti wa Taifa wa Wafanyabiashara, Mwenyekiti wa wafanyabiashara Kariakoo, na Wafanyabiashara wengine ni Ismail Masoud Kutoka Tanga, Fred Ngajiro (Vunja Bei) Awadh Mpandira, Salome Mgaya (Mama Bonge), na Omari Hussein kutoka Zanzibar.
Katika hatua nyingine Mheshimiwa Majaliwa amesema Rais wa Serikali ya Awamu ya Sita Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan anathamini Sekta ya Biashara na ameagiza kufanya maboresho kuanzia Wafanyabiashara wadogo hadi wakubwa ili kukuza Sekta hiyo.
“Serikali yetu ya awamu ya sita chini ya Rais wetu, itaendelea kuimarisha Biashara zenu, kilio chenu tumekisikia, na ndiyo maana nimerudi tena kwa maelekezo ya Rais wetu, naomba muone nia ya dhati ya Serikali yenu kwamba mfanye Biashara zenu na mpate mafanikio”.
Aidha, Mheshimiwa Majaliwa ameiagiza kamati aliyounda kufanya mapitio ya madai ya Wafanyabiashara ambao mizigo yao imekamatwa na kuwasilisha mapendekezo kwa Kamishna wa TRA ili waone uwezekano wa kuiachia kwa kutengeneza unafuu kwa wafanyabiashara.
“Kamishna wa TRA, mizigo imekaa sana na mingine imeshuka thamani, uking’ang’ania ulipwe kodi ile ile hutapata chochote itaharibika, kaangalie utaratibu mwingine nafuu.”
Akihitimisha mazungumzo na Wafanyabiashara hao, Mheshimiwa Majaliwa amewasihi Wafanyabiashara hao kuendelea na Biashara zao.
“Nawasihi mrudi kazini ili mkafanye Biashara, kwa niaba ya Rais Samia Suluhu Hassan naomba mridhie kufungua Maduka ili tunusuru soko la kimataifa liendelee kuwa na heshima yake.”
PIA UNAWEZA KUSOMA👇
- TETESI za Usajili NBC Premier League 2023/2024
- YANGA yashika Nafasi ya 9 Simba ya 10 Afrika 2022/2023
- FAHAMU kuhusu Azam Pesa pamoja na Makato yake
- Ada mpya za M-Pesa 2023/2024 | Makato mapya ya M-Pesa
- DOWNLOAD | NYIMBO ZA TENZI ZA ROHONI SWAHILI MIX
- Ada za M-Pesa Songesha 2022/2023
- FAHAMU Jinsi ya Kufungua Akaunti ya M-Koba Vodacom
- Namna ya Kujisajili na Premier Bet Ushinde Mamilioni
- RATIBA kamili NBC Premier League msimu wa 2022/2023
- DOWNLOAD NIDA number | Kitambulisho cha Taifa
- MSIMAMO Ligi Kuu Tanzania Bara 2022/2023
- WAFUNGAJI Wanaoongoza kwa Ufungaji Ligi Kuu
Nijuze TV ni App ambayo ukiwa nayo utaweza kutazama mechi za Ligi Kuu Tz Bara (NBC PREMIER LEAGUE) EPL, WORLD CUP, EPL, LALIGA, SERIA, LIGUE 1, BUNDESLIGA na Ligi nyingine nyingi.
Download App ya Nijuze Habari Playstore tukutumie Habari zote kwenye Simu yako BILA MALIPO BOFYA HAPA.
Download App ya Nijuze TV Utazame mechi zote kwenye Simu yako BOFYA HAPA
Tags: KAMATI ya watu 14 yaundwa kutatua mgogoro wa Wafanyabiashara Kariakoo