MFANO wa Barua ya kuomba kazi Sheli
JIUNGE NA GROUP LETU LA WHATSAPP HAPA
JIUNGE NA CHANNEL YETU YA TELEGRAM HAPA
AJIRA MPYA ZA WIKI HII BONYEZA HAPA
AUDIOS MPYA ZA WIKI BONYEZA HAPA
VIDEOS MPYA ZA WIKI HII BONYEZA HAPA
MFANO wa Barua ya kuomba kazi Sheli

MFANO wa Barua ya kuomba kazi Sheli
MFANO wa Barua ya kuomba kazi Sheli, Kwa mujibu wa mitandao mingi ya Kijamii, kuomba Kazi Sheli hakuna vigezo zaidi ya kujuana na watu wanaofanya Kazi hiyo.
Au kama una ndugu yako anamiliki Sheli unamuomba anakupachika tu wala hatokuomba vyeti vyako, au kama una jamaa, rafiki anafanya Kazi Sheli unamuomba akufanyie Connection ya kukuweka hapo au akuconnect kwenye Sheli zingine ambazo kuna marafiki zake au ndugu.
Lazima uwe na connection na hiyo na huyo mtu akubali kukudhamini. Maana bila mdhamin kuipata hiyo Kazi ni vigumu.
Aidha Kazi ya Sheli ni nzuri kwa mtu mvumilivu asiye na tamaa ya maisha, Kazi ya Sheli ina changamoto ya kushika Pesa nyingi kwa siku, kwani unaweza kuuza hadi milioni 5-6 na zaidi, mshahara laki na nusu kwa mwezi.
Pengine kuna bonasi ukiuza kila Lita moja unapata Tsh 2, kwa hiyo ukiuza Lita 10,000 inazidishwa Mara Tsh 2 ndiyo inakuwa bonasi yako na inaongezwa kwenye mshahara.
Lakini kuna short kIla siku ambazo hazikwepeki hata kwa wale wazoefu, ambapo hiyo hasara hukatwa kwenye mshahara wako wa mwisho wa mwezi.
kila unapouza Lita zako unaandika na shoti yako unaandika kila siku ya kazi mwisho wa mwezi wanajumlisha jumla ya Lita ulizouza wanazidisha Mara sh 2 ya bonus ya Kila Lita wanatoa kwa shoti zako zote za mwezi mzima, unapewa mshahara wako,ukipiga shoti nyingi ndivyo mshahara wako unavyopungua.
Mfano, ukijisahau ukafanya mistake yeyoyote kama kuweka petrol kwenye gari la dizel, wewe ndiye utalipa utaelewana na mwenye gari, ukisahau kuchukua hela ukampa mtu mafuta bure utakatwa kwenye mshahara wako mwisho wa mwezi hata iwe mafuta ya milioni unalipa.
Aidha kazi hii kama sehemu ya magari mengi wanawake ndiyo hufaidika sana, maana unatakiwa uchangamke kuita magari ukizembea utauza laki na mwenzako atauzabmilioni na zaidi, hata madereva wengi wanawake kwa wanaume hasa madereva wa malori wanapenda kuhudumiwa na wanawake.
Unaweza jiuliza ni kwa nini sheli nyingi wahudumu ni wanawake, jibu ni kuwa pale kuna Pesa nyingi inaingia kwa siku hivyo wanawake ni dhaifu akipewa Mshahara wa laki na nusu (150,000) anaridhika, lakini mwanaume saa yeyote anapindua meza.
Kupata kazi ya sheli mpaka connection, uwe na mtu wa karibu anaefanya kazi sheli au anayefahamiana kiukaribu zaidi na mameneja au wafanyakazi, hizo kazi ni kushikana mikono tu, hakuna vigezo.
Hayo maelezo ya juu ni kwa mujibu Wa kituo kimoja Jijini Dar es salaam, sijui kampuni zingine zinautaratibu gani, ila nikutie moyo usikate tamaa endelea kutafuta kazi hii utapata.
Unaweza kutumia barua hii kuomba Kazi sehemu yoyote na ukakubaliwa kwa urahisi.
- Anuani ya mwandishi, yaani anuani yako wewe unayeandika barua hiyo.
- Tarehe.
- Anuani ya anayeandikiwa.
- Salamu.
- Kichwa cha habari.
- Kiini cha barua.
Hii ni roho ya barua yako, ukikosea mahali hapa, kama unajibu swali katika mtihani utapoteza alama, na kama unaomba kazi halisi utaikosa.
Kiini kina aya nne:
- Katika aya ya kwanza, eleza kazi unayoomba na mahali ulipoona tangazo la kazi hiyo, ni katika sehemu hii unaweza kutaja umri wako.
- Katika aya ya pili, eleza ujuzi wako kwa ufupi, usieleze sana, Barua hii haipaswi kuwa ndefu kupindukia.
- Aya ya tatu eleza kwa nini upewe kazi hii wewe na si mtu mwingine, Epuka kueleza shida zako binafsi ili upewe kazi. Maneno kama, ninaomba kazi hii ili niweze kumtibia mama yangu mgonjwa kitandani, hayana msaada wowote.
- Aya ya nne eleza uko tayari kwa usahili siku gani?
- Mwisho wa barua.
Mwisho wa barua yako uwe na:
- Neno la kufungia. Wako mtiifu. Wako katika ujenzi wa taifa n.k
Pia, barua ya maombi ya kazi, huambatana na CV, hivyo utakapomaliza kujifunza jinsi ya kuandika barua ya maombi ya kazi, tafadhali jifunze hapa jinsi ya kuandika CV.
MKWANJA Mrefu Upo Premierbet Leo, kupata odds za Kibabe Tafadhali Bofya HAPA JISAJILI, BASHIRI Utusue.
Karibu Helabet Upige MKWANJA hadi 300,000, Kujiunga Bofya HAPA, Promo Code ya Bonasi Weka NIJUZE, JISAJILI, Deposit na Utusue.
Simu: 0759895821,
Barua Pepe: [email protected],
DAR ES SALAAM.
09/03/2023.
Mkurugenzi Mkuu,
Shirika la Reli Tanzania,
S.L.P 76956,
DAR ES SALAAM.
Ndugu,
Yah: OMBI LA KAZI YA FUNDI UMEME
Mimi ni Mwanamume mwenye umri wa miaka 30, ninaomba Kazi ya Fundi Umeme kama ilivyotangazwa na Shirika la Reli Tanzania siku ya tarehe 28/02/2023 katika Tovuti, mitandao ya Kijamii na mbao za matangazo.
Nina Cheti cha Fundi Umeme nilichotunukiwa kutoka VETA mwaka 2022, pia nina uzoefu wa kufanya kazi na nimefanya kazi na Taasisi ya Century Holding Company Limited.
Kutokana na Elimu yangu, uwezo wa kufanya kazi nilio nao, uzoefu, pamoja na kuwa na sifa zinazotakiwa, ninaamini kuwa ninastahili kupata kazi hii.
Endapo nitapata kazi hii ya Fundi Umeme, nitafanya kazi kwa bidii kama ilivyoelekezwa, baadhi ya majukumu yangu ni;
- Kutengeneza mifumo ya umeme
- Kuhakikisha vifaa vya umeme vinafanya kazi na kufuata maelekezo nitakayopangiwa.
Nipo tayari kwa usaili siku yoyote nitakayohitajika, vilevile ninatarajia majibu mazuri kutoka kwako na nimeambatanisha nakala ya vyeti vyangu kwa uthibitisho zaidi.
Wako mtiifu,
CV au wasifu ni kitu cha lazima kwa yeyote anayeomba kazi. Watu wengi wanaokosa kazi, tatizo huwa siyo wao, bali tatizo huwa ni CV zao.
Kumekuwa na makosa mengi katika uandishi wa CV jambo ambalo limesababisha watafuta kazi wengi kushindwa kuitwa kwenye usaili.
Makala hii itakueleza namna sahihi ya kuandika CV, utaitwa katika ‘interview’ nyingi endapo utaandika CV sahihi.
Tena nakukumbusha, kila taaluma ina aina yake ya CV, CV ya rubani haifanani na CV ya injinia, vivyo hivyo CV ya mpishi haifananani na CV ya Mwalimu.
Pia nakukumbusha usome jinsi ya kuandika barua ya maombi ya kazi, kwani CV huenda pamoja na barua ya maombi ya kazi.
Mfano wa CV ya Kiswahili
WASIFU WA SAMWEL MANATI MALUMBAGA
Taarifa za Awali
Jina: Samwel Manati Malumbaga
Ndoa: Ameoa
Barua Pepe: [email protected]
Simu: 0754 89 53 21
Utaifa: Mtanzania
Tarehe ya kuzaliwa: 02/08/1989
- Historia ya Elimu
2007-2008, VETA Dodoma.
2013-2016, Shule ya Sekondari Kiwanja cha Ndege. Cheti cha Kidato cha Nne.
19966-2012, Shule ya Msingi Makole. Cheti cha Darasa la Saba.
- Uzoefu
2012-2013, Mgodi wa Bulyanhulu.
- Maarifa
Kutumia Kompyuta.
- Ninapenda
Kufanya kazi, Kufundisha, Kusoma, Kujifunza mambo mapya.
- Wadhamini:
1:Mwalimu Makoba
Barua Pepe: [email protected]
Contact: 0754 89 53 21
Dar es Salaam.
- David Mwakimonga,
Mkufunzi,
Chuo Kikuu cha Dar es Salaam,
S.L.P 35040,
Dar es Salaam.
MFANO wa Barua ya kuomba kazi Sheli, Barua ya kuomba kazi kiswahili,Jinsi ya kufanya kazi sheli,Mshahara wa sheli,Kazi ya kuuza mafuta sheli,Nafasi za kazi Sheli 2023,Barua za maombi ya kazi kwa kiswahili,Jinsi ya Kuandika Barua ya kuomba kazi (Mifano),Namna ya kuandika barua ya kuomba kazi inayojitosheleza vizuri,Naomba ufafanuzi kuhusu kazi za vituo vya kuuza mafuta, Nafasi za kazi sheli |Ajira za kuuza Mafuta Sheli, Fahamu Utaratibu wa Kuomba Leseni ya Biashara ya Kituo cha mafuta,FAHAMU JINSI KUANDIKA BARUA RASMI,Mfano wa Barua ya Kuomba Kazi/Maombi ya Kazi,Leo nimekusogezea Mfano wa Barua ya maombi ya kazi kwa kiswahili,Jinsi ya Kuandika Barua ya Maombi ya Kazi Mwaka 2023.

Download App ya Nijuze Habari Playstore tukutumie Habari zote kwenye Simu yako BILA MALIPO BOFYA HAPA.
Tags: Barua ya kuomba kazi kiswahili, Barua za maombi ya kazi kwa kiswahili, FAHAMU JINSI KUANDIKA BARUA RASMI, Fahamu Utaratibu wa Kuomba Leseni ya Biashara ya Kituo cha Mafuta, Jinsi ya Kuandika Barua ya kuomba kazi (Mifano), Jinsi ya Kuandika Barua ya Maombi ya Kazi Mwaka 2023., Jinsi ya kufanya kazi sheli, Kazi ya kuuza mafuta sheli, Leo nimekusogezea Mfano wa Barua ya maombi ya kazi kwa kiswahili, MFANO wa Barua ya kuomba kazi Sheli, Mfano wa Barua ya Kuomba Kazi/Maombi ya Kazi, Mshahara wa sheli, Nafasi za kazi sheli |Ajira za kuuza Mafuta Sheli, Nafasi za kazi Sheli 2023, Namna ya kuandika barua ya kuomba kazi inayojitosheleza vizuri, Naomba ufafanuzi kuhusu kazi za vituo vya kuuza mafuta