NANI Kumrithi Robertinho Simba (Sven van Denbroeck/Abdelhak)
JIUNGE NA GROUP LETU LA WHATSAPP HAPA
JIUNGE NA CHANNEL YETU YA TELEGRAM HAPA
AJIRA MPYA ZA WIKI HII BONYEZA HAPA
AUDIOS MPYA ZA WIKI BONYEZA HAPA
VIDEOS MPYA ZA WIKI HII BONYEZA HAPA
NANI Kumrithi Robertinho Simba (Sven van Denbroeck/Abdelhak)

NANI Kumrithi Robertinho Simba (Sven van Denbroeck/Abdelhak)
NANI Kumrithi Robertinho Simba (Sven van Denbroeck/Abdelhak), Mtendaji Mkuu wa Simba Imani Kajula, amesema kuwa klabu hiyo iko kwenye hatua za mwisho kukamilisha mchakato wa kupatikana kocha mpya ambaye atarithi mikoba iliyoachwa wazi na Robertinho Olivera aliyefutwa kazi wiki iliyopita.
Akizungumza katika tukio la uzinduzi wa Channel ya WhatsApp ya Simba SC, Kajula aliwatoa hofu Wanasimba akibainisha kuwa wamebakisha hatua chache kukamilisha mchakato huo.
Taarifa za uhakika kutoka ndani ya uongozi wa Simba zinabainisha kuwa majina ya makocha wawili Sven van Denbroeck na Abdelhak Benchikha mmoja anaweza kupewa mikoba hiyo.
MKWANJA Mrefu Upo Premierbet Leo, kupata odds za Kibabe Tafadhali Bofya HAPA JISAJILI, BASHIRI Utusue.
Karibu Helabet Upige MKWANJA hadi 300,000, Kujiunga Bofya HAPA, Promo Code ya Bonasi Weka NIJUZE, JISAJILI, Deposit na Utusue.
Simba ilifanya mazungumzo na makocha wote ambao kimsingi wako tayari kubeba majukumu ya kuinoa Simba na hatua iliyobaki ni uongozi kuamua nani akabidhiwe mikoba kwa kutegemea na mahitaji yao na mikakati wanayokuja nayo.
Kocha Mkuu anatarajiwa kuja na Kocha Msaidizi ikimaanisha kuwa Kocha Seleman Matola atarejea kwenye majukumu yake ya kuzinoa timu za vijana na Daniel Cadena akiendelea na majukumu ya ukufunzi wa magolikipa.
Aidha Sven ana faida ya kuifahamu vyema Simba na Ligi Kuu ya Tanzania Bara baada ya kuwa amefanya kazi hapo karibu misimu miwili awali na kushinda mataji yote ya ndani.
Pamoja na hilo pia wachezaji wengi ambao wako Simba alifanya nao kazi awali na hivyo kama atapata nafasi ya kuifundisha Simba ni wazi ana pa kuanzia.
Kwa upande wa Benchikha ni kocha mwenye mafanikio katika ngazi ya mashindano ya CAF, msimu uliopita akiisaidia USM Alger kufika Fainali na kushinda taji la Shirikisho (CAF CC) dhidi ya Yanga SC.
Pia mwanzoni mwa msimu aliiongoza USM Alger kutwaa Super Cup baada ya ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Al Ahly.
NANI Kumrithi Robertinho Simba (Sven van Denbroeck/Abdelhak)

Download App ya Nijuze Habari Playstore tukutumie Habari zote kwenye Simu yako BILA MALIPO BOFYA HAPA.

Tags: NANI Kumrithi Robertinho Simba (Sven van Denbroeck/Abdelhak)