Ruvu Shooting yashuka Daraja 2022/2023

AJIRA MPYA ZA WIKI HII BONYEZA HAPA
AUDIOS MPYA ZA WIKI BONYEZA HAPA
VIDEOS MPYA ZA WIKI HII BONYEZA HAPA


Ruvu Shooting yashuka Daraja 2022/2023

Ruvu Shooting yashuka Daraja 2022/2023
KICHAPO Cha Mabao 3-0 ilichokipata Ruvu Shooting kutoka kwa Simba SC, katika mchezo uliopigwa uwanja wa Azam Complex, Jijini Dar es salaam Jana May 12,2023 kimeifanya timu hiyo kushuka Daraja hadi Championship kimahesabu.
Mabao ya Simba kwenye mchezo huo yalifungwa na Clatous Chama dakika ya 30 na Pape Sakho aliyefunga mawili dakika ya 72 na 90.
Matokeo hayo yanamaanisha Ruvu Shooting imeipa mkono wa kwa heri Ligi Kuu ya NBC (NBC Premier League 2022/2023) kuelekea mechi mbili za mwisho.
Ruvu Shooting imebakiwa na mechi mbili mkononi ambazo hata ikishinda itafikisha pointi 26 ambazo ni pungufu kwa Mbeya City iliyopo nafasi ya 14 na pointi 27 ikiwa imebakiza mechi tatu tu.

Ruvu Shooting yashuka Daraja 2022/2023
Kwa maana matokeo yeyote itakayoyapata Ruvu katika mechi mbili zilizosalia hayataivusha katika nafasi mbili za mkiani kwa maan ya nafasi ya 16 na 15 hivyo inashuka daraja moja kwa moja.
Ikumbukwe moja ya sheria za Ligi Kuu ni kushuka daraja moja kwa moja kwa timu mbili zitakazomaliza mkiani huku zile zitakazoishia nafasi za 13 na 14 kuamuliwa na mechi za mtoano ‘Play Off’.
Mechi mbili za mwisho za Ruvu itacheza na timu za kanda ya kati kwa maana ya Singida Big Stars iliyojihakikishia kumaliza katika nafasi nne za juu kwenye Msimamo pamoja na Dodoma Jiji inayohaha kutocheza Play Off.
Ushindi huo unaifanya Simba kufikisha pointi 67 baada ya kucheza Michezo 28, nyuma ya Mabingwa watetezi, Young Africans wenye pointi 71 baada ya kucheza Michezo 27, ikisalia katika nafasi ya pili, ikiwa imebakiwa na mechi mbili dhidi ya Coastal Union na Polisi Tanzania.
Katika hatua nyingine Klabu ya Young Africans inaweza kutawazwa Mabingwa kwa msimu wa pili mfululizo endapo watashinda mchezo wa leo dhidi ya Dodoma Jiji, kwani itafikisha pointi 74 ambazo haziwezi kufikishwa na Simba anayefuata kwenye nafasi ya Pili hata akishinda mechi zake mbili zilizobaki.
PIA UNAWEZA KUSOMA👇
- FAHAMU kuhusu Azam Pesa pamoja na Makato yake
- Ada mpya za M-Pesa 2023/2024 | Makato mapya ya M-Pesa
- DOWNLOAD | NYIMBO ZA TENZI ZA ROHONI SWAHILI MIX
- Ada za M-Pesa Songesha 2022/2023
- FAHAMU Jinsi ya Kufungua Akaunti ya M-Koba Vodacom
- MFUMO wa maombi ya Kitambulisho cha Taifa (NIDA) Online
- JINSI ya kupata mikopo ya vijana na wanawake
- Namna ya Kujisajili na Premier Bet Ushinde Mamilioni
- RATIBA kamili NBC Premier League msimu wa 2022/2023
- DOWNLOAD NIDA number | Kitambulisho cha Taifa
- MSIMAMO Ligi Kuu Tanzania Bara 2022/2023
- WAFUNGAJI Wanaoongoza kwa Ufungaji Ligi Kuu
Nijuze TV ni App ambayo ukiwa nayo utaweza kutazama mechi za Ligi Kuu Tz Bara (NBC PREMIER LEAGUE) EPL, WORLD CUP, EPL, LALIGA, SERIA, LIGUE 1, BUNDESLIGA na Ligi nyingine nyingi.