Sababu za Saido kubaki Dar zatajwa

AJIRA MPYA ZA WIKI HII BONYEZA HAPA
AUDIOS MPYA ZA WIKI BONYEZA HAPA
VIDEOS MPYA ZA WIKI HII BONYEZA HAPA


Sababu za Saido kubaki Dar zatajwa

Sababu za Saido kubaki Dar zatajwa
Klabu ya Simba SC, leo alfajiri imesafiri kuelekea nchini Guinea kwaajili ya mchezo wa kwanza wa kundi C Klabu Bingwa Afrika dhidi ya Horoya Athletic Club.
Mchezo huo unatarajiwa kufanyika Jumamosi ya February 11, 2023 kuanzia saa 1:00 Usiku kwenye Uwanja wa General Lansana Conte.
Kuelekea mchezo huo Simba itaikosa huduma ya Kiungo wao Mshambuliaji, Saido Ntibazonkiza ambaye hakuwa sehemu ya Kikosi kilichoifuata Horoya AC.
Baada ya kumtafuta Daktari wa Simba, Edwin Kagabo amesema kuwa Saido anaendelea vizuri na killichomfanya kutokuwa kwenye kikosi kinachosafiri ni kutokana na kutofanya mazoezi pamoja na wenzake.
Kagabo amefafanua kuwa Saido alipata maumivu ya nyama za paja katika mchezo dhidi ya Singida Big Stars, na hali yake imeimarika lakini hawezi kusafiri kwa kuwa hayuko timamu na hajafanya mazoezi na wenzake.
Daktari huyo ameongeza kuwa timu hiyo ikirejea nchini Saido atajiunga na Wachezaji wenzake kwaajili ya maandalizi ya michezo inayofuata.
Baada ya kurejea nchini Klabu ya Simba itaanza maandalizi ya mchezo wa pili wa Kundi C dhidi ya Raja Casablanca utakaopigwa February 18, 2023 kwenye Uwanja wa Benjamin Mkapa Jijini Dar es salaam.
- SHINDA MAMILIONI NA GAL SPORT TANZANIA, JISAJILI HAPA KUSHINDA
- MATOKEO ya Kidato cha Nne 2022/2023
- RATIBA kamili ya hatua ya 16 Bora Azam Sports Federation Cup 2023
- RATIBA kamili NBC Premier League msimu wa 2022/2023
- DOWNLOAD NIDA number | Kitambulisho cha Taifa
- MSIMAMO Ligi Kuu Tanzania Bara 2022/2023
- WAFUNGAJI Wanaoongoza kwa Ufungaji Ligi Kuu
- RATIBA ya Yanga CAF Confederation Cup 2022/2023 hatua ya Makundi
- RATIBA ya Simba CAF Champions League hatua ya Makundi
Nijuze TV ni App ambayo ukiwa nayo utaweza kutazama mechi za Ligi Kuu Tz Bara (NBC PREMIER LEAGUE) EPL, WORLD CUP, EPL, LALIGA, SERIA, LIGUE 1, BUNDESLIGA na Ligi nyingine nyingi.