LIVE USM ALGER VS YANGA Download HAPA kutazama LIVE kwenye Simu Yako Kesho Saa 4:00 Usiku.

LIVE MAN CITY VS MAN UNITED Download HAPA kutazama LIVE kwenye Simu Yako Kesho Saa 11:00 Jioni.

Sakho aitwa timu ya Taifa Senegal

Filed in Michezo by on 17/03/2023 0 Comments
Share This
NIJUZE HABARI WHATSAPP GROUP

AJIRA MPYA ZA WIKI HII BONYEZA HAPA


AUDIOS MPYA ZA WIKI BONYEZA HAPA


VIDEOS MPYA ZA WIKI HII BONYEZA HAPA

Nijuze TV App, Mpira Kiganjani Mwako

Sakho aitwa timu ya Taifa Senegal

Sakho aitwa timu ya Taifa Senegal

Sakho aitwa timu ya Taifa Senegal

Kwa mara ya kwanza tangu alipojiunga na Simba SC mwanzoni mwa msimu uliopita, Kiungo Mshambuliaji wa Senegal, Pape Osmane Sakho ametajwa kwenye kikosi cha Timu ya Taifa ya Senegal.DROO ya Robo na Nusu Fainali UEFA Champions League 2022/2023

Kocha Mkuu wa timu ya Taifa ya Senegal, Khalou Cisse amemtaja kiungo huyo katika kikosi chake ambacho mwishoni mwa wiki ijayo kitacheza dhidi ya Msumbiji katika kusaka nafasi ya kushiriki Fainali za Mataifa ya Afrika ‘AFCON 2023’.

Sakho aitwa timu ya Taifa Senegal

Sakho aitwa timu ya Taifa Senegal

Sakho ambaye ni mfungaji wa goli bora la Afrika mwaka jana anakuwa mchezaji pekee kutoka Afrika kuitwa kwenye kikosi cha Taifa cha Senegal na Aliou Cisse.

Baada ya kumaliza mchezo wa kesho wa Marudiano wa Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya Horoya, Sakho atapata ruhusa ya kwenda kujiunga na Simba hao wa Terenga.

Nyota wengine wa kimataifa wa Simba SC walioitwa timu zao Taifa ni:

Henock Inonga (DR Congo), Clatous Chama (Zambia) na Peter Banda (Malawi).

Kwa upande wa Yanga wameitwa Kipa Djigui Diarra (Mali), Khalid Aucho (Uganda), Stephane Aziz Ki (Burkina Faso), Kennedy Musonda (Zambia) na Fiston Kalala Mayele (DRC).

Kutoka Azam FC wameitwa Ali Ahmada (Comoro) na Kenneth Muguna (Kenya).

KMC wameitwa Emmanuel Mvuyekure na Steve Nzigamasabo (Burundi) na Coastal Union ameitwa kipa Justin Ndikumana (Burundi).

Aidha kutoka Singida Big Stars ameitwa Meddie Kagere kikosi cha timu ya Taifa ya Rwanda.

Sakho kutoka Simba SC ya Tanzania anaungana na Wachezaji wengine wanaocheza katika nafasi za Ushambuliaji walioitwa katika kikosi hicho kama Nahodha Sadio Mane kutoka Bayern Munich, Boulaye Dia kutoka Salerntana, Habib Diallo kutoka Strasbourg, Bamba Dieng kutoka Lorient na Iliman Ndiaye kutoka Sheffield United.

Wachezaji wengine walioitwa kwenye kikosi cha Senegal upande wa Walinda Lango ni Seny Dieng (Opr), Alfred Gomis (Como) na Mory Diaw (Clermont)

Mabeki: Youssouf Sabaly (Betis Seville), Noah Fadiga (Brest), Kalidou Koulibaly (Chelsea), Formose Mendy (Amiens), Abdoulaye Seck (Maccabi), Moussa Niakhate (Nottingham), Ismail Jakobs (Monaco) na Abdallah Ndour (Sochaux)

Viungo: Gana Gueye (Everton), Nampalys Mendy (Leicester), Pape Gueye (Seville), Pathe Ciss (Vallecano), Pape Matar Sarr (Tottenham) Na Dion Lopy (Reims)

Senegal itacheza dhidi ya Msumbiji mjini Dakar kwenye Uwanja wa Diamniadio Olympic Machi 24, kisha itacheza ugenini mjini Maputo katika Uwanja wa do Zimpeto, Machi 28,2023.

Senegal inaongoza Msimamo wa Kundi L ikiwa na pointi 6, ikifuatiwa na Msumbiji yenye pointi 4, Rwanda ipo nafasi ya tatu ikiwa na pointi 1 huku Benin ikiwa mkiani baada ya kupoteza michezo yote hadi sasa.

Nijuze TV ni App ambayo ukiwa nayo utaweza kutazama mechi za Ligi Kuu Tz Bara (NBC PREMIER LEAGUE) EPL, WORLD CUP, EPL, LALIGA, SERIA, LIGUE 1, BUNDESLIGA na Ligi nyingine nyingi.

Download App ya Nijuze Habari Playstore tukutumie Habari zote kwenye Simu yako BILA MALIPO BOFYA HAPA.

Download App ya Nijuze TV Utazame mechi zote kwenye Simu yako BOFYA HAPA

Share This

Tags:

About the Author ()

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *