Sandaland amrithi Vunjabei Simba SC
JIUNGE NA GROUP LETU LA WHATSAPP HAPA
JIUNGE NA CHANNEL YETU YA TELEGRAM HAPA
AJIRA MPYA ZA WIKI HII BONYEZA HAPA
AUDIOS MPYA ZA WIKI BONYEZA HAPA
VIDEOS MPYA ZA WIKI HII BONYEZA HAPA
Sandaland amrithi Vunjabei Simba SC

Sandaland amrithi Vunjabei Simba SC
Sandaland amrithi Vunjabei Simba SC, Klabu ya Simba umefikia makubaliano ya kuingia mkataba mpya wa miaka miwili wa kutengeneza na kusambaza jezi na Kampuni ya Sandaland Fashion Wear Limited.
Mkataba huo umesainiwa jana Jijini Dar es Salaam baada ya klabu hiyo kumalizana na Kampuni ya Vunja Bei iliyoingia mkataba miaka miwili iliyopita ukiwa na thamani ya Sh 2 Bilioni.
Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano ya Simba, Ahmed Ally, alisema kuwa, wameamua kuingia mkataba na Sandaland baada ya kuvutiwa na ofa yao iliyokuwa mara mbili na ile iliyopita ya Vunja Bei.
“Tunajivunia kwa kupata mkataba huu ambao utakuwa ni wa kutengeneza na kusambaza jezi za timu zetu. Ilikuwa ngumu kukataa ofa hii ya Sandaland na utakuwa wa miaka miwili na kila msimu itakuwa ni Sh 2 Bilioni, ikiwa na maana kwa miaka miwili klabu inavuna Sh 4 Bilioni,” alisema Ally.
Kulingana na Mkataba huo, Sandaland wamepewa haki ya kuisimamia Simba kwenye matukio yake ya kimichezo ikiwa ni pamoja na kuhamasisha mashabiki kununua jezi na kwenda uwanjani na Mkurugenzi wa kampuni hiyo, Yusuf Omar Yenga aliwaahidi wanachama, Mashabiki na Wapenzi wa Simba kuwa watashuhudia jezi zenye ubora na zitakazopatikana kwa haraka kwani kwa sasa mzigo upo njiani unakuja.
“Tunawaahidi mashabiki kupata jezi zenye ubora na zitakazopatikana kwa wakati kabla hata ya Tamasha ya Simba Day, kwa vile mzigo kwa sasa upo njiani na tumejipanga kuusambaza mapema na kumfikia kila Mwanasimba,” alisema Yenga aliyefafanua kuwa wameanza kupokea oda za mawakala mikoani ili mzigo ukija usambazwe kuwawezesha wanasimba kupata jezi kirahisi popote walipo.
Yenga aliongeza kywa Sandaland ina maduka makubwa mawili ya kuuza jezi Jijini Dar es Salaam ambayo itawarahisisha wanachama, mashabiki na wapenzi wa Simba kupata jezi za msimu ujao kirahisi, huku wale wa mikoani watapata kwa mawakala watakaojiorodhesha na kuweka oda zao kuanzia sasa.
Kwa upande wa CEO, Imani Kajula alisema iuwa Simba haiwezi kuwa timu kubwa Afrika bila kuwa na uwezo wa kifedha, “leo hii tunasimamia sana kwenye eneo hilo. Kwetu hatua ni safari na leo tunapiga hatua kubwa zaidi.”
“Mashabiki walitwambia wanataka tuwe na jezi bora, zifike kwa wakati na zipatikane kila sehemu.”
“Mwanzoni tulikuwa tunapata milioni 400 kwa mwaka kutokana na jezi. Akaja Vunja Bei akatupa bilioni moja kwa mwaka na huyu wa sasa anakuja kutupa bilioni mbili kwa mwaka. Namshukuru sana Sandaland kuwa mdhamini wa jezi kwa msimu wa 2023/24.
Mwenyekiti wa Bodi Salim Abdallah ‘Try Again’ yeye aliwapongeza Sandaland kwa kupata nafasi hii, alisema kuwa Sandaland alijaribu mara ya kwanza hakufanikiwa lakini muda huu amepata. Namshukuru pia VunjaBei kwa udhamini aliotupatia.”
MKWANJA Mrefu Upo Premierbet Leo, kupata odds za Kibabe Tafadhali Bofya HAPA JISAJILI, BASHIRI Utusue.
Karibu Helabet Upige MKWANJA hadi 300,000, Kujiunga Bofya HAPA, Promo Code ya Bonasi Weka NIJUZE, JISAJILI, Deposit na Utusue.
“Tunajipanga kusajili timu yenye ubora na usajili unakwenda vizuri. Simba inakwenda kuondoa unyonge, Simba ijayo.
Baadhi ya wadau wa habari wakizungumzia mkataba wa udhamini wa jezi ambao Simba imeingia na Sandaland The Only One.
Sandaland amrithi Vunjabei Simba SC,Sandaland amrithi Vunjabei Simba,Simba Sc yaingia mkataba wa Sh bil 4 na Sandaland kutengeneza jezi zake,Sandaland yachukua nafasi za Vunjabei Simba Sc,Mrithi Wa Vunjabei Simba ni Sandaland, Thanks you Vunjabei, Welcome Sandaland Simba.
PIA UNAWEZA KUSOMA👇
- Ada/makato ya Lipa kwa M-pesa, Lipa kwa Simu
- ADA za LIPA kwa Airtel Mitandao Yote
- TETESI za Usajili NBC Premier League 2023/2024
- YANGA yashika Nafasi ya 9 Simba ya 10 Afrika 2022/2023
- FAHAMU kuhusu Azam Pesa pamoja na Makato yake
- Ada mpya za M-Pesa 2023/2024 | Makato mapya ya M-Pesa
- Ada zaAirtel Money 2022/2023 | Makato mapya ya Airtel Money
- ADA Mpya za Tigo Pesa (Tigo Pesa Tariffs 2022/2023)
- Ada/Makato ya HaloPesa Tanzania, Halopesa Tariffs 2023
- DOWNLOAD | NYIMBO ZA TENZI ZA ROHONI SWAHILI MIX
- Ada za M-Pesa Songesha 2022/2023
- FAHAMU Jinsi ya Kufungua Akaunti ya M-Koba Vodacom
- Namna ya Kujisajili na Premier Bet Ushinde Mamilioni
- RATIBA kamili NBC Premier League msimu wa 2022/2023
- DOWNLOAD NIDA number | Kitambulisho cha Taifa
- MSIMAMO Ligi Kuu Tanzania Bara 2022/2023
- WAFUNGAJI Wanaoongoza kwa Ufungaji Ligi Kuu
Nijuze TV ni App ambayo ukiwa nayo utaweza kutazama mechi za Ligi Kuu Tz Bara (NBC PREMIER LEAGUE) EPL, WORLD CUP, EPL, LALIGA, SERIA, LIGUE 1, BUNDESLIGA na Ligi nyingine nyingi.

Download App ya Nijuze Habari Playstore tukutumie Habari zote kwenye Simu yako BILA MALIPO BOFYA HAPA.

Tags: Mrithi Wa Vunjabei Simba ni Sandaland, Sandaland amrithi Vunjabei Simba, Sandaland amrithi Vunjabei Simba SC, Sandaland yachukua nafasi za Vunjabei Simba Sc, Simba Sc yaingia mkataba wa Sh bil 4 na Sandaland kutengeneza jezi zake, Thanks you Vunjabei, Welcome Sandaland Simba.