TETESI za Usajili Barani Ulaya Leo Jumatano 24 May 2023

AJIRA MPYA ZA WIKI HII BONYEZA HAPA
AUDIOS MPYA ZA WIKI BONYEZA HAPA
VIDEOS MPYA ZA WIKI HII BONYEZA HAPA


TETESI za Usajili Barani Ulaya Leo Jumatano 24 May 2023

TETESI za Usajili Barani Ulaya Leo Jumatano 24 May 2023
Klabu ya Arsenal ipo tayari kuuza wachezaji wanane wa kikosi cha kwanza msimu huu, huku kiungo wa kati wa Leicester City na Muingereza James Maddison, mwenye umri wa miaka 26, na kiungo wa kati wa West Ham ya Uingereza Declan Rice mwenye umri wa miaka 24, wakiwa miongoni mwa wachezaji wapya wanaopania kuwasajili. (Mirror)
The Gunners pia ina nia ya kumnunua kiungo wa kati wa Ujerumani Ilkay Gundogan ikiwa mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 32 hatakubali kusaini mkataba mpya na Manchester City. (ESPN)
Mshambulizi wa Ajax Amstadam na Ghana, Mohammed Kudus mwenye umri wa miaka 22, ambaye amekuwa akihusishwa na Arsenal, Manchester United na Newcastle United, amekataa kuongezwa kwa mkataba katika klabu hiyo na wakala wake anaamini “sasa ni wakati mwafaka” kwa mchezaji huyo kuondoka. (De Telegraaf – kwa Kiholanzi)
Klabu ya Everton inapanga kumuuza kiungo wa kati wa Ubelgiji, Amadou Onana mwenye umri wa miaka 21, kwa £60m ili kufadhili mipango yao ya uhamisho wa majira ya joto. (Football Insider)
Beki wa Ufaransa, Jules Kounde ameiambia Barcelona kwamba anataka kuondoka katika klabu hiyo msimu wake wa joto, hata hivyo timu hiyo ya La Liga itazingatia tu ofa za euro 80m (£69.4m) kwa mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 24. (Sport – kwa Kihispania)
Mshambulizi wa Ureno, Cristiano Ronaldo anataka kuondoka katika klabu ya Al Nassr ya Saudi Arabia na huenda akarejea tena Ulaya. (Mundo Deportivo – kwa Kihispania)
Klabu ya Juventus imesema kuwa haina nia ya kumuuza Mshambuliaji wa Serbia, Dusan Vlahovic mwenye umri wa miaka 23 baada ya kukatwa pointi katika hatua ambayo huenda ikaifanya klabu hiyo kukosa nafasi ya kucheza Ligi ya Mabingwa. (90 Min)
Klabu ya Fenerbahce ya Ururuki, inaongoza katika kinyang’anyiro cha kumsajili mshambuliaji wa Ubelgiji, Divock Origi kutoka AC Milan, ambayo iko tayari kumuuza Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 28 mwaka mmoja tu baada ya kujiunga kutoka Liverpool. (Calciomercato – kwa Kiitaliano)
Klabu ya Real Madrid imemuongeza nahodha wa Liverpool na Scotland, Andy Robertson mwenye umri wa 29, kwenye orodha ya Wachezaji wanaoweza kuchukua nafasi ya beki wa Ufaransa Ferland Mendy mwenye umri wa miaka 27. (Mail).
Klabu ya Bayern Munich inamlenga Mshambuliaji wa Manchester City na Argentina, Julian Alvarez mwenye umri wa miaka 23 kwenye usajili wa majira ya joto. (Bild – kwa Kijerumani)
Klabu ya Manchester United inafikiria kuwasajili washambuliaji wawili wapya wa kati – lakini wasiafikiane na Tottenham kuhusiana na usajili wa nahodha wa Uingereza, Harry Kane mwenye umri wa miaka 29. (90min).
PIA UNAWEZA KUSOMA👇
- Ada/makato ya Lipa kwa M-pesa, Lipa kwa Simu
- ADA za LIPA kwa Airtel Mitandao Yote
- TETESI za Usajili NBC Premier League 2023/2024
- YANGA yashika Nafasi ya 9 Simba ya 10 Afrika 2022/2023
- FAHAMU kuhusu Azam Pesa pamoja na Makato yake
- Ada mpya za M-Pesa 2023/2024 | Makato mapya ya M-Pesa
- Ada zaAirtel Money 2022/2023 | Makato mapya ya Airtel Money
- ADA Mpya za Tigo Pesa (Tigo Pesa Tariffs 2022/2023)
- Ada/Makato ya HaloPesa Tanzania, Halopesa Tariffs 2023
- DOWNLOAD | NYIMBO ZA TENZI ZA ROHONI SWAHILI MIX
- Ada za M-Pesa Songesha 2022/2023
- FAHAMU Jinsi ya Kufungua Akaunti ya M-Koba Vodacom
- Namna ya Kujisajili na Premier Bet Ushinde Mamilioni
- RATIBA kamili NBC Premier League msimu wa 2022/2023
- DOWNLOAD NIDA number | Kitambulisho cha Taifa
- MSIMAMO Ligi Kuu Tanzania Bara 2022/2023
- WAFUNGAJI Wanaoongoza kwa Ufungaji Ligi Kuu
Nijuze TV ni App ambayo ukiwa nayo utaweza kutazama mechi za Ligi Kuu Tz Bara (NBC PREMIER LEAGUE) EPL, WORLD CUP, EPL, LALIGA, SERIA, LIGUE 1, BUNDESLIGA na Ligi nyingine nyingi.
Download App ya Nijuze Habari Playstore tukutumie Habari zote kwenye Simu yako BILA MALIPO BOFYA HAPA.
Download App ya Nijuze TV Utazame mechi zote kwenye Simu yako BOFYA HAPA
Tags: TETESI za Usajili Barani Ulaya Leo Jumatano 24 May 2023