TETESI za Usajili NBC Premier League 2023/2024
JIUNGE NA GROUP LETU LA WHATSAPP HAPA
JIUNGE NA CHANNEL YETU YA TELEGRAM HAPA
AJIRA MPYA ZA WIKI HII BONYEZA HAPA
AUDIOS MPYA ZA WIKI BONYEZA HAPA
VIDEOS MPYA ZA WIKI HII BONYEZA HAPA
TETESI za Usajili NBC Premier League 2023/2024
TETESI za Usajili NBC Premier League 2023/2024, Tetesi za Usajili NBC Premier League Tanzania 2023/2024,Dondoo na tetesi za Usajili Ligi Kuu Tanzania Bara 2023/2024,Tetesi za Usajili NBC Premier League,Tetesi za Usajili Tanzania 2023/2024 NBC Premier League.

Ayoub Lakred Simba SC
Klabu ya Simba imefikia Makubaliano ya kumsajili aliyekuwa Kipa wa FAR Rabat ya Morocco, Ayoub Lakred mwenye umri wa miaka 28 kama Mbadala wa Jefferson Luis aliyeondolewa kambini nchini Uturuki kutokana na majeraha ya muda mrefu.
Klabu ya Tabora United imemtambulisha Nyota wa kimataifa wa DR Congo, Lumiere Banza Kalumba akitokea klabu ya TP Mazembe.
klabu ya KMC FC imekamilisha usajili wa Issa Ndala kutoka Azam FC kwa mkopo wa msimu mmoja.
Klabu ya Ihefu Fc imewatambulisha wachezaji wawili ambao ni beki wa kulia wa Paul Godfrey “Boxer” kutoka Singida Fountain Gate pamoja na Ezekia Mwashilindi kutoka Tanzania Prisons.
Klabu ya Geita Gold imekamilisha usajili wa beki wa kulia Mwita Gereza, Ihefu pia Imekamilisha usajili wa Mshambuliaji Ismail Mgunda kutoka Tanzania Prisons.
Klabu ya Mashujaa Imekamilisha usajili wa Mshambuliaji, Hussein Mwaterema kwa mkataba wa mwaka mmoja kutoka Dodoma Jiji FC.
Klabu ya Kagera Sugar Imekamilisha usajili wa Gaspaer Mwaipas kwa mkataba wa miaka miwili.
Klabu ya Geita Gold imekamilisha usajili wa George Sangija kutoka Mbeya City.
Klabu ya Mashujaa imekamilisha usajili wa beki, Juma Said Makapu kutoka Ihefu SC.
Klabu ya Tabora United imekamilisha usajili wa kiungo, Mutuale Nyongani Junior kutoka Maniema Union Fc kwa mkataba wa mwaka mmoja.
Klabu ya Tabora United imethibitisha kumuongeza mkataba mpya wa mwaka mmoja nahodha wao, Said Mbatty.
Klabu ya Tabora United imemtambulisha, Lumiere Banza Kalumba kutoka TP Mazembe ya kwao DR Congo.

Hussein Abel Simba SC
Klabu ya Simba imetangaza kukamilisha Usajili wa mlinda mlango, Hussein Abel kutoka KMC FC.
Klabu ya Geita Gold imekamilisha usajili wa beki wa kulia wa zamani wa Kagera Sugar FC, Mwita Gereza.
Klabu ya Ihefu Imekamilisha usajili wa Mshambuliaji wa zamani wa Tanzania Prisons, Ismail Mgunda.
Gael Bigirimana anatarajiwa kutolewa kwa mkopo na klabu yake ya Yanga SC kabla ya dirisha la usajili wa ndani halijafungwa August 31.2023.
Klabu ya Kagera Sugar Imekamilisha usajili wa Mshambuliaji wa zamani wa Yanga na Azam FC, Obrey Chirwa kwa mkataba wa miaka 2 akiwa mchezaji huru kutoka Ihefu SC
Klabu ya Kagera Sugar Imekamilisha usajili wa kiungo, Nicholas Kasoz kwa mkataba wa miaka 2 akitokea KCCA ya kwao Uganda.
Klabu ya Mtibwa Sugar leo imekamilisha usajili wa kiungo Mshambuliaji, Haruna Kassim Shaban “Tiote” kutoka Namungo FC kwa mkataba wa miaka miwili.
Klabu ya Mtibwa Sugar Imekamilisha usajili wa Mshambuliaji wa zamani wa Dodoma Jiji FC, Seif Kalihe.
Klabu ya Ihefu SC imefikia makubaliano ya kumsajili moja kwa moja kwa mkataba wa mwaka mmoja Kiungo, Victor Akpan baada ya kuachana Simba SC.
Klabu ya Kagera Sugar Imekamilisha usajili wa Mshambuliaji, Abiud Khabely kutoka Mashujaa FC kaka Mchezaji huru kwa mkataba wa miaka 2.
Klabu ya Ihefu SC, imefikia makubaliano ya kumuongezea mkataba mpya wa mwaka Mshambuliaji wake Yacouba Sogne.
Kiungo wa Mtibwa Sugar, Baraka Gamba Majogoro amejiunga na Klabu ya Chipa United ya nchini Africa Kusini kwa mkataba wa miaka mitatu baada ya kufuzu majaribio.
Aliyewahi kuwa kocha Msaidizi wa Simba SC na kocha mkuu wa Dodoma Jiji, Masoud Djuma Irambona leo ametambulishwa rasmi kuwa kocha Mkuu wa klabu ya KMKM ya visiwani Zanzibar’
Klabu ya Mtibwa Sugar Imekamilisha usajili wa beki wa pembeni, Yassin Mustapha pamoja na Abal Kassim Suleiman kutoka Singida Big Stars FC kwa mkataba wa miaka miwili.
Klabu ya Kagera Sugar Imekamilisha usajili wa Mshambuliaji wa zamani wa Atlabara FC ya Sudani Kusini, Dickson Gidion kwa mkataba wa miaka miwili.
Klabu ya Tanzania Prisons imekamilisha usajili wa Mshambuliaji, Eliud Ambokile kutoka Mbeya City iliyoshuka Daraja.
Klabu ya Mtibwa Sugar Imekamilisha usajili wa Mshambuliaji, Juma Luizio kutoka Geita Gold FC ya Geita.
Klabu ya KMC imekamilisha usajili wa kiungo, Ibrahim Mao kutoka Kibra United ya nchini Kenya kwa mkataba wa miaka miwili.
Klabu ya Singida Fountain Gate FC imekamilisha Usajili wa Mshambuliaji, Thomas Ulimwengu kutoka TP Mazembe ya DR Congo.
Klabu ya KMC FC imekamilisha usajili wa beki wa kulia, Rogars Gabriel kutoka Pamba FC ya Mwanza.
Klabu ya Coastal Union imekamilisha usajili wa kiungo Mshambuliaji, Lucas Kikoti kutoka Namungo FC.
Klabu ya Coastal Union FC imekamilisha usajili wa Kiungo, Abrahim Ajibu kutoka akitokea Singida Fountain Gate FC.
Klabu ya Tabora United (Kitayose FC) imetangaza kumsajili Mlinda mlango John Noble raia wa Nigeria mwenye umri wa miaka 30 kutoka klabu ya Enyimba ya Nigeria kwa mkataba wa mwaka mmoja.
Hata hivyo klabu ya Simba iliingilia kati dili hilo Kwaajili ya saini yake ili kuziba pengo la Jefferson Luis raia wa Brazil ambaye amepata majeraha ya muda mrefu na hayupo kwenye mipango ya Klabu hiyo kuelekea msimu mpya wa 2023/2024.

Jefferson Luis Szerban de Oliveira Junior Simba SC
Klabu ya Simba SC imeachana na golikipa wao mpya Jefferson Luis raia wa Brazil kutokana na golikipa huyo kuumia mazoezini hivo atakuwa nje ya uwanja kwa muda mrefu

John Noble Barinyima Simba SC
Kutokana na hilo Simba inafanya mazungumzo na golikipa wa klabu ya Enyimba ya Nigeria, John Noble Barinyima kwaajili ya kuziba nafasi ya Jefferson kabla ya dirisha la usajili halijafungwa kesho Jumatatu saa 6:00 usiku.

Hafiz Konkoni Yanga SC
Klabu ya Young Africans imetangaza kukamilisha Usajili wa Mshambuliaji, Hafiz Konkoni raia wa Ghana kwa mkataba wa miaka miwili.
Mshambuliaji huyo mwenye umri wa miaka 23 kutoka timu ya Bechem United FC inayoshiriki Ligi Kuu ya Ghana ndiye mrithi wa Fiston Kalala Mayele aliyeuzwa Pyramids FC ya Misri.

Yanick Bangala Azam FC
Klabu ya Azam FC imekamilisha usajili wa Mchezaji Kiraka, Yanick Bangala mwenye umri wa 29 kutoka Yanga kwa mkataba wa miaka miwili

Pape Osmane Sakho Quevilly Rouen Metropole (QRM)
Klabu ya Simba SC, imefikia makubaliano na klabu ya Quevilly Rouen Metropole (QRM) ya nchini Ufaransa kumnunua Kiungo Mshambuliaji Kutoka Senegal Pape Osmane Sakho.

Emmanuel Mahop Dikongue Yanga SC
Klabu ya Yanga SC imefikia makubaliano ya kumsajili Mshambuliaji, Emmanuel Mahop Dikongue mwenye umri wa miaka 28 kutoka klabu ya FC Conan Younde ya kwao Cameroon kwa mkataba wa miaka miwili.

Hussein Kazi Simba SC
Klabu ya Simba SC imekamilisha usajili wa mlinzi wa kati, Hussein Kazi mwenye umri wa miaka 23 kutoka Geita Gold kwa mkataba wa miaka miwili.

Shaban Idd Chilunda Simba SC
Klabu ya Simba imekamilisha usajili wa Mshambuliaji, Shaban Idd Chilunda mwenye umri wa miaka 25 kutoka Azam FC kwa mkataba wa miaka miwili akiwa mchezaji huru.

Abdallah Hamis Simba SC
Klabu ya Simba imekamilisha usajili wa usajili wa kiungo mkabaji, Abdallah Hamis kama mchezaji huru kwa Mkataba wa miaka miwili.

Shabani Idd Chilunda Simba SC
Klabu ya Simba SC, imekamilisha Usajili wa Mshambuliaji, Shabani Idd Chilunda kama Mchezaji huru kutoka Azam FC kwa mkataba wa miaka miwili.
Klabu ya Supersport United ya Africa kusini imekamilisha usajili wa Mchezaji, Abdulrazack Hamza kutoka Namungo FC.
Klabu ya Mashujaa imekamilisha usajili wa Mfungaji Bora wa Ligi Kuu ya Vijana U20, Athuman Masumbuko (Mang’ombe) kutoka Mtibwa Sugar FC.

Peter Banda Simba SC
Klabu ya Simba SC, inatarajiwa kumtoa kwa mkopo kiungo Mshambuliaji wake kutoka Malawi Peter Banda.
Pape Osmane Sakho anatajwa kutokuwa sehemu ya kikosi cha Simba SC kwa msimu ujao wa 2023/2024.

Pape Osmane Sakho Simba SC
Klabu ya Mashujaa FC ya Kigoma, imekamilisha usajili wa Mshambuliaji, Onesmo Mayaya kutoka Mtibwa Sugar FC.

Shabani Msala akijaribu kumtoka aliyekuwa kiongo wa Simba na sasa Singida Fountain Gate FC, Said Khamis Ndemla
Klabu ya Ihefu SC, imepanga kuwabakisha Wachezaji wake Yacouba Sogne pamoja na Juma Nyoso, Ihefu pia imekamilika usajili wa kiungo, Shabani Msala kutoka Ruvu Shooting FC pamoja Geoffrey Manyasi kutoka Geita Gold FC.
Klabu ya JKT Tanzania FC, imekamilisha usajili wa nyota wa zamani wa Vilabu vya Alliance, Polisi Tanzania na Geita Gold Cosmas Okoyo.
Klabu ya Ihefu SC, imekamilisha usajili wa beki wa Kati, Vedastus Mwhihambi kutoka Mtibwa Sugar kwa mkataba wa miaka miwili.

Tuisila Rossien Kisinda Mashujaa FC
Klabu ya Mashujaa FC imetuma maombi ya kutaka kumsajili winga, Tuisila Kisinda kwa mkopo kutoka RS Berkane ya Morocco.
Klabu ya Tanzania Prisons imekamilisha usajili wa Mchezaji, Salum Kihimbwa kutoka Mbeya City.

Zouzoua Pacome Yanga SC
Klabu ya Yanga imekamilisha Usajili wa Kiungo, Zouzoua Pacome mwenye umri wa miaka 26 ambaye ndiye Mchezaji Bora wa ASEC Mimosas wa msimu uliopita wa 2022/2023 akiwashinda Kwame Kramo wa Simba, Mohammed Zoungrana na Yaou Kouas Attohoula wa Yanga.

Luis Jose Miquissone Simba SC
Klabu ya Al Ahly ya Misri imefikia makubaliano ya kuvunja mkataba na Kiungo Mshambuliaji, Luis Jose Miquissone kwa makubaliano ya pande zote mbili, ni rasmi Miquissone maarufu ‘Konde Boy’ anarejea Simba SC kama Mchezaji huru akitokea Abha FC ya Saudi Arabia alipokuwa kwa mkopo.

Medjo Simon Loti Omossola Simba SC
Klabu ya Simba ipo katika mpango wa kuinasa saini ya Golikipa wa zamani wa Vilabu vya AS Vita Club na Cotton Sport, Medjo Simon Loti Omossola raia wa Cameroon mwenye umri wa miaka 25, kutoka Saint Lupopo ya DR Congo.

Mahlatse Makudubela Skudu Young Africans SC
Klabu ya Yanga SC imefikia makubaliano ya kumsajili winga, Mahlatse Makudubela Skudu raia wa Afrika Kusini mwenye umri wa miaka 33 kutoka Marumo Gallants ya Afrika Kusini kwa mkataba wa mwaka mmoja kama Mchezaji huru.

Clatous Chama Simba SC
Uongozi wa klabu ya Simba SC umemalizana na kiungo, Clatous Chama baada ya kufikia makubaliano ya kuongeza mkataba mpya wa mwaka mmoja ambao utamfanya aendelee kuwatumikia Simba hadi Julai mwa 2025.
kwa sasa Chama ataelekea nchini Uturuki kujiunga na kikosi cha Simba kwaajili ya maandalizi ya msimu mpya 2023/2024.

Fiston Mayele Pyramids FC
Klabu ya Pyramids FC ya Misri imefikia makubaliano na Yanga ya kumsajili Mshambuliaji wa Kimataifa wa DR Congo, Fiston Mayele.

Fiston Kalala Mayele Yanga SC
Uongozi wa Klabu ya Yanga umetajwa kufikia Makubaliano ya kumuuza Mshambuliaji wao, Fiston Mayele baada ya nyota huyo kuonyesha nia ya kutaka kuondoka Klabuni hapo.

Fiston Kalala Mayele Yanga
Mayele ambaye ni Mfungaji Bora wa Ligi Kuu msimu uliopita wa 2022/2023 akifunga mara 17, ametajwa kuhitajika na timu za AL Qadisiyah ya Saudi Arabia na Pyramids ya Misri.

Luis Jose Miquissone Simba SC
Klabu ya Simba SC, imetajwa kukamilisha taratibu zote za kumrejesha fundi mwenye kasi na chenga nyingi, mbishi mpambanaji wa Msumbiji, Luis Jose Miquissone kutoka Abha FC ya Saudi Arabia alipokuwa kwa mkopo kutoka Al Ahly ya Misri.
Klabu ya Geita Gold imekamilisha usajili wa Mshambuliaji, Valentino Mashaka kutoka Ruvu Shooting ya Pwani.
Klabu ya Geita Gold FC imekamilisha usajili wa Mshambuliaji, Tariq Seif kutoka Polisi Tanzania iliyoshuka Daraja.
Baada ya mkataba wa msimu mmoja aliosaini akitokea Azam FC, Kiungo Never Tigere raia wa Zimbabwe ameongeza mkataba mpya wa kuendelea kuitumikia Ihefu SC.
Klabu ya Kagera Sugar FC imekamilisha usajili wa beki, Mohamed Mussa kutoka visiwani Zanzibar katika Klabu ya KVZ kwa mkataba wa miaka 2
Klabu ya West Armenia inayoshiriki Ligi Daraja la Kwanza la nchini Armenia imekamilisha usajili wa Mchezaji Abal Kassim kutoka Ruvu Shooting ya Pwani.
Klabu ya Kagera Sugar imefikia makubaliano binafsi na nyota wa Mbeya City, Richadson N’godya.
Klabu ya Dodoma Jiji imekamilisha usajili wa kiungo, Gustapha Simon kutoka Coastal Union ya Tanga.
Klabu ya Singida FG Fc Imekamilisha usajili wa kiungo, Morice Chukwu kwa mkataba wa miaka 2 akitokea River United ya kwao Nigeria.

Kouassi Attohoula Yao Yanga SC
Klabu ya Yanga imekamilisha Usajili wa Mlinzi wa Kulia, Kouassi Attohoula Yao mwenye umri wa miaka 26 kutoka ASEC Mimosas ya Ivory Coast.

Farbice Luamba Ngoma Simba SC
Klabu ya Simba SC imemtambulisha Kiungo, Farbice Luamba Ngoma kutoka Al Hilal ya Sudan kuwa mchezaji wao mpya kuelekea msimu ujao wa 2023/2024.

Maxi Mpia Nzengeli Yanga SC
Klabu ya Yanga imemtambulisha winga Maxi Mpia Nzengeli kutoka AS Maniema Union ya kwao DR Congo kuwa mchezaji wake mpya wa nne kuelekea msimu mpya wa 2023/2024.

Maxi Mpia Nzengeli Yanga SC
Klabu ya Yanga Imefikia Makubaliano ya kununua mkataba wa mwaka 1 uliosalia wa winga huyo raia wa DR Congo, Maxi Mpia Nzengeli mwenye umri wa miaka 23 kutoka Maniema FC ya kwao.

Jonas Gerlad Mkude Yanga SC
Klabu ya Yanga SC imetaganza kukamilisha usajili wa kiungo Mkabaji, Jonas Gerlad Mkude kama mchezaji huru baada ya kumaliza mkataba wake na klabu ya Simba SC.

Mohammed Hussein Zimbwe Simba SC
Mlinzi wa Kushoto wa Klabu ya Simba SC, Mohammed Hussein Zimbwe amesaini mkataba wa miaka miwili wa kuendelea kuichezea klabu hiyo mkataba ambao utaisha July 2025.

David Kameta ‘Duchu’ Simba SC
Mlinzi wa kulia, David Kameta ‘Duchu’ amesaini mkataba mpya wa miaka mitatu kuendelea kusalia katika kikosi cha Simba SC akitokea Mtibwa Sugar alipokuwa kwa mkopo.

Shomari Salum Kapombe Simba SC
Mlinzi wa kulia wa Klabu ya Simba SC, Shomari Salum Kapombe ameongeza mkataba wa miaka miwili kuitumikia Simba SC hadi Julai 2025.
Klabu ya Kagera Sugar FC ipo kwenye mazungumzo na Gasper Mwaipas akiwa mchezaji huru baada ya mkataba wake na Mbeya City kumalizika.

Maxi Mpia Nzengeli Yanga SC
Klabu ya Yanga SC imefikia makubaliano ya kumsajili winga, Maxi Mpia Nzengeli mwenye umri wa miaka 23 kutoka klabu ya Maniema Union ya nchni kwao DR Congo kwa mkataba wa miaka miwili.

Gift Fred Yanga SC
Klabu ya Young Africans imefikia Makubaliano ya kumsajili Beki wa kati wa timu ya taifa ya Uganda, Gift Fred kwa mkataba wa miaka mitatu kama Mchezaji huru baada ya mkataba wake na SC Villa.

Che Fondoh Malone Simba SC
Klabu ya Simba imekamilisha usajili wa Beki, Che Fondoh Malone mwenye umri wa miaka 24 kutoka Coton Sport FC ya kwao Cameroon.

Joash Onyango Singida Fountain Gate FC
Klabu ya Singida Fountain Gate FC imekamilisha usajili wa Beki, Joash Onyango raia wa Kenya kutoka Simba SC.
Onyango mwenye umri wa miaka 30 amesaini mkataba wa miaka miwili kuitumikia Singida Fountain Gate FC hadi July 2026.

Aubin Kramo Kouamé Simba SC
Klabu ya Simba SC, imetangaza kukamilisha usajili wa kiungo mshambuliaji Aubin Kramo Kouamé kutoka Asec Mimosas ya kwao Ivory Coast.

Leandre Willy Essomba Onana Simba SC
Klabu ya Simba SC imetangaza kukamilisha usajili wa winga, Leandre Willy Essomba Onana raia wa Cameroon mwenye umri wa miaka 23 kutoka Rayon Spots ya Rwanda kwa mkataba wa miaka miwili.

Nickson Clement Kibabage
KLABU ya Yanga imetangaza kukamilisha usajili wa beki, Nickson Kibabage kutoka Singida Big Stars kwa mkataba wa miaka miwili utakaomalizika 2026.

Fabrice Ngoma Simba SC
Klabu ya Simba SC imefanya mazungumzo ya kumsajili kiungo, Fabrice Ngoma raia wa DR Congo mwenye umri wa miaka 29 kutoka Al Hilal ya Sudani.
Ngoma aliandika barua ya kuomba kuvunja mkataba wake na klabu yake ya Al Hilal ya kutokana na machafuko ya kisiasa nchini humo.

Cheikh Tidiane Sidibe Azam FC
KLABU ya Azam FC imetangaza kukamilisha Usajili wa beki wa kushoto, Cheikh Tidiane Sidibe kutoka Teungueth ya kwao Senegal.

Hassan Saleh Dilunga JKT Tanzania FC
Kiungo wa zamani wa vilabu vya JKT Ruvu, Mtibwa Sugar, Yanga sc na Simba sc Hassan Dilunga ametajwa kujiunga na JKT Tanzania FC iliyopanda Ligi Kuu ya NBC 2023/2024 kwa mkataba wa miaka miwili.

Idris Mbombo Azam FC
Mshambuliaji wa Azam FC, Idris Mbombo ameongeza mkataba mpya wa mwaka mmoja kuendelea kubakia ndani ya viunga vya Azam Complex hadi mwaka 2025.

Abdallah Kheri ‘Sebo’ Azam FC
Beki wa Azam FC, Abdallah Kheri ‘Sebo’ ameongeza mkataba miaka miwili kuendelea kubakia ndani ya viunga vya Azam Complex hadi mwaka 2026.

Gibril Sillah Azam FC
Klabu ya Azam Fc imekamilisha usajili wa kiungo Gibril Sillah, raia wa Gambia mwenye umri wa miaka 24 akitokea JS Soualem alipokuwa kwa mkopo kutoka Raja Casablanca ya Morocco.

Jonas Gerald Mkude Yanga SC
Baada ya kuitumikia klabu ya simba kwa takribani miaka 13 hatimaye Jonas Mkude amejiunga na Yanga Sc kwa mkataba wa msimu mmoja.

George Amani Mpole Kitayosce FC
Klabu ya Kitayosce FC ya Tabora ipo kwenye Mazungumzo na klabu ya Fc Lupopo ili kumsajil mshambuliaji wa zamani wa Geita Gold ya Geita, George Mpole kwa mkopo.

Nickson Kibabage Yanga SC
Klabu ya Yanga SC imefikia makubaliano ya kumsajili beki wa kushoto wa Singida Fountain Gate FC ya Singida, Nickson Kibabage kwa mkataba wa miaka mitatu.

Pape Malickou Ndoye Azan FC
Beki wa Azam FC, Pape Malickou Ndoye ameongeza mkataba mpya wa mwaka mmoja kuendelea kubakia ndani ya viunga vya Azam Complex hadi mwaka 2025.

Daniel Amoah Azam FC
Beki wa kati wa Azam FC Daniel Amoah ameongeza mkataba mwaka mmoja kuendelea kubakia ndani ya viunga vya Azam Complex hadi mwaka 2025.

Aziz Andambwile Singida Fountain Gate FC
Klabu ya Singida Fountain Gate FC imemuongezea mkataba wa miaka mitatu kiungo wake, Aziz Andambwile utakaomalizika June 2026.

Caique Luiz Santos de Purificacao Simba SC
Klabu ya Simba SC ipo kwenye mazungumzo ya usajili na golikipa Caique Luiz Santos de Purificacao mwenye umri wa miaka 25 kutoka Ypiranga FC ya kwao Brazil

Clatous Chama Simba SC
Klabu ya Simba SC imefikia makubaliano na Mchezo Clatous Chama raia wa Zambia ya kumuongeza mkataba mpya wa miaka miwili.

Mamadou Douambia Simba SC
Klabu ya Yanga huenda ikaachana na beki wao Mamadou Douambia raia wa Mali.

David Kakolanya Azam FC
Baada ya kuachana na simba SC, aliyekuwa golikipa nambari mbili Beno David Kakolanya anatarajiwa kujiunga na Azam FC.

Kibu Denis Simba SC
Mshambuliaji wa klabu ya Simba SC, Kibu Dennis amefikia makubaliano ya kuongeza mkataba mpya na klabu hiyo utakaomalizika June 2025

Bruno Gomes Barroso Singida Fountain Gate FC
Klabu ya Singida Fountain Gate Fc ya Singida imethibitisha kumuongeza mkataba mpya wa miaka 2 kiungo wake Bruno Gomes Barroso raia wa Brazil mwenye umri wa miaka 26, mkataba huo utakaomalizika juni 2025.

Yusufu Kagoma Singida Fountain Gate FC
Klabu ya Singida Fountain Gate imemuongeza mkataba kiungo wake, Yusuph Kagoma utakaomfanya aendelee kusalia kwa walima alizeti hao wa hadi 2026.
MKWANJA Mrefu Upo Premierbet Leo, kupata odds za Kibabe Tafadhali Bofya HAPA JISAJILI, BASHIRI Utusue.
Karibu Helabet Upige MKWANJA hadi 300,000, Kujiunga Bofya HAPA, Promo Code ya Bonasi Weka NIJUZE, JISAJILI, Deposit na Utusue.
Klabu ya Yanga imethibitisha kuachana na Abdallah Shaibu (Ninja)
Beki kulia, Nathanael Chilambo atasalia Azam FC hadi mwaka 2025, baada ya Kusaini mkataba mpya wa miaka miwili.

Crysin Ngushi Kitayosce FC
Klabu ya Kitayosce FC (Tabora United) ipo kwenye mazungumzo na Mshambuliaji wa Yanga Crysin Ngushi ambaye mkataba wake umefikia tamati.
Klabu ya Dodoma Jiji Imekamilisha usajili wa wachezaji wawili, ambao ni kiungo Gustapha Simon na Winga Idd Kipagwile.
Klabu ya Coastal Union imethibitisha kuachana na wachezaji wake wawili ambao ni Yusuph Athuman pamoja na Yusuph Jamali Kisongo.
Klabu ya Namungo imethibitisha kuachana na wachezaji 7, ambao Chareli, Bressing, Smith, Farjala, Yangson, Bwenzi na Abdulrazack.

Milton Karisa Simba SC
Klabu ya Simba tayari imetuma ofa ya kutaka kumsajili winga wa kimataifa wa Uganda na Vipers SC, Milton Karisa mwenye umri wa miaka 27.
Klabu ya Namungo FC ya Ruangwa Mkoani Lindi imetaganza kumsajili beki Erasto Edward Nyoni kutoka klabu ya Simba SC.
Klabu ya Azan Fc imethibitisha kumuongeza mkataba mpya kiungo wao James Akaminko utakaomalizika juni 2026.
Mshambuliaji wa Azam Fc Prince Dube amesaini mkataba mpya wa miaka 3 wa kuendelea kuitumikia timu hiyo hadi juni 2026.
Klabu ya Azam FC imethibitisha kumuongeza mkataba mpya wa miaka 3 Sospeter Bajana utakaomfanya aendelee kusalia katika viunga vya Azam Fc hadi mwaka 2026.
Uongozi wa Klabu ya Yanga sc umepanga kumuongeza mkataba mpya wa mwaka mmoja winga wao Jesus Moloko
Danny Lyanga, D. Okoyo, Tariq Seif na Ismail Aziz wote wamejiunga na Klabu ya JKT Tanzania iliyopanda daraja msimu huu wa 2023/2024.
Cleophace Mkandala amejiunga na Kagera Sugar FC ya Kagera akitokea Azam FC.
Uongozi wa Klabu ya KMC upo kwenye mazungumzo na kocha wao mkuu Jamhuri Kiwelu ili kumuongeza mkataba mpya baada ya aliokuwa amesaini kumalizika mwishoni mwa msimu huu.
KMC pia ipo kwenye mazungumzo na beki wa pembeni wa Yanga, David Brayson baada ya mkataba wake na Yanga kumalizika.
Klabu ya Yanga sc imethibitisha kuachana na nyota wao Dickson Ambundo na Benard Morrison.
Klabu ya Coastal Union imethibitisha kuachana na nyota wao raia wa Uganda Joseph Zziwa pamoja na beki wao wa pembeni Emery Nimubona raia wa Burundi pia Coastal Union imeachana na golikipa wao Mahmoud mroville raia wa Comoro
Klabu ya simba imethibitisha kuachana na kiungo wao Victor Akpan raia wa Nigeria, Simba pia imeachana na golikipa Beno Kakolanya, wengine ambao Simba imeachana nao ni Jonas Mkude, Mohamed Quatara, Erasto Nyoni na Nelson Okwa,
Klabu ya Coastal Union imethibitisha kuachana na wachezaji wao wawili ambao ni Djibril Naim Olatoudji pamoja na Geurold Mwamba wa Mwamba
Uongozi wa Klabu ya Yanga sc umepanga kumuongeza mkataba mpya wa mwaka mmoja winga wao Jesus Moloko.

Sadio Kanoute Simba SC
Simba pia ipo kwenye mazungumzo ya kumuongeza mkataba mpya kiungo wake Sadio Kanoute raia wa Mali mwenye umri wa miaka 26.

Joyce Lomalisa Azam FC
Klabu ya Azam FC ipo kwenye mpango wa kumsajili beki wa kushoto, Joyce Lomalisa kutoka Yanga SC.

Joash Onyango Simba SC
Uwezekano wa beki wa Kati kutoka Kenya, Joash Onyango kusalia Msimbazi msimu ujao wa 2023/24 unazidi kuwa mdogo baada ya beki huyo kuendelea na Msimamo wake wa kutaka kuondoka Klabuni hapo.

Tariq Seif Mbeya City FC
Klabu ya JKT Tanzania ipo kwenye mazungumzo na Tariq Seif Kiakala Kutoka Mbeya City pamoja na Deusdedity Cosmas Okoyo kutoka Geita Gold FC.

Dany Lyanga Geita Gold FC
Vilabu vya Dodoma Jiji, Namungo FC na JKT Tanzania vinahaha kuinasa saini ya Mshambuliaji wa Geita Gold, Dany Lyanga

Philippe Kinzumbi and Aubin Kouame Kramo Young Africans SC
Majina yana Philippe Kinzumbi kutoka TP Mazembe pamoja na Aubin Kouame Kramo kutoka ASEC Mimosas ni Miongoni mwa majina yaliyopo kwenye orodha ya Wachezaji watakaosajiliwa na Yanga sc msimu ujao wa 2023/204.

Ismail Aziz Kada
Baada ya kuachana na klabu ya Azam FC Ismail Aziz Kada huenda akajiunga na JKT Tanzania iliyopanda Ligi Kuu ya NBC msimu huu wa 2023/24 kwa mkataba wa miaka 2.

Jean Othos Balake Simba SC
Uongozi wa Klabu ya Simba upo Kwenye Mazungumzo na TP Mazembe ili kumsajili Mshambuliaji wao, Jean Balake moja kwa moja ambaye amebakiza mkataba wa mkopo wa mwaka mmoja.

Leandre Essomba Willy Onana Simba SC
Klabu ya Simba SC, imekamilisha usajili wa Winga Leandre Essomba Willy Onana raia wa Cameroon mwenye umri wa miaka kutoka Rayon Sports ya Rwanda kwa mkataba wa miaka miwili.

Adel Zrane Simba SC
Simba pia imefanikiwa kumresha Adel Zrane ambaye ni fitness Coach akichukuwa nafasi ya Kelvin Mandla aliyeana na Simba hivi Karibuni.

Cheikh Sidibe Azam FC
Klabu ya Azam FC kwenye hatua za mwisho kukamilisha Usajili wa beki wa kushoto wa timu ya Taifa ya Senegal na Teungueth, Cheikh Sidibe mwenye umri wa miaka 24, ili kuziba pengo la Bruce Kangwa ambaye huenda akaachwa

Feisal Salum Abdallah
Klabu ya Azam FC, imekamilisha usajili wa Kiungo Feisal Salum Abdallah ‘Fei toto’ kutoka Young Africans kwa mkataba wa miaka mitatu (3).

Makabi Lilepo Simba SC
Klabu ya Simba imetajwa kupeleka ofa ya kuhitaji saini ya Mshambuliaji wa Al Hilal ya Sudan, Makabi Lilepo kwa mkopo na golikipa Issa Fofana kwa mkataba wa moja kwa moja.

Fabrice Ngoma Young Africans
Baada ya kuvunja mkataba wake na Al Hilal ya Sudan, Fabrice Ngoma raia wa DR Congo anatajiwa kuitumikia Young Africans msimu ujao wa 2023/2024.

Willy Esomba Onana Simba SC
Usajili wa Willy Esomba Onana kwenda Simba SC kutoka Rayon Sports na Coulibaly Wanlo kutoka ASEC Mimosas upo Katika hatua za mwisho.

Lamine Jarjou Azam FC
Klabu ya Azam FC ipo kwenye mpango wa kuhakikisha wanainasa saini ya Mshambuliaji wa Al Hilal ya Sudan, Lamine Jarjou mwenye umri wa miaka 21 raia wa Gambia kwa mkopo wa mwaka mmoja.

Yahya Zayd Azam FC
Klabu ya Azam FC inatajiwa kuachana na Wachezaji Yahya Zayd, Cleophace Mkandala, Bruce Kangwa, Ismail Aziz Kada na Wilbol Maseke Changarawe.

Dickson Ambundo Young Africans
Dickson Ambundo huenda akarejea Dodoma Jiji FC baada ya mkataba wake na Young Africans kumalizika mwishoni mwa msimu huu wa 2022/2023.

Hassan Kessy Mtibwa Sugar
Klabu hiyo ya Jijini Dodoma huenda ikaachana na Beki wa Kulia Hassan Kessy na Aman Kyata mwishoni mwa msimu huu wa 2022/2023.
Hassan Maulid Machezo Simba SCKlabu ya Simba imetajwa kuwa katika hatua za mwisho kukamilisha Usajili wa kiungo Hassan Maulid Machezo kutoka Mbeya City, kwaajili ya kuziba pengo la Jonas Mkude, ambaye inadaiwa Simba wana mpango wa kuachana naye mwisho wa msimu huu wa 2023/2024.

Yusufu Kagoma & Jonas Mkude Singida Big Stars FC
Kuna uwezekano makubwa wa Yusufu Kagoma kuondoka Singida BS mwishoni nwa msimu huu na nafasi yake kuchukuliwa na Jonas Mkude kutoka Simba SC.

Coulibaly Wanlo Simba SC
Klabu ya Simba inatajwa kuiwinda saini ya beki wa kati, Coulibaly Wanlo mwenye umri wa miaka 31 kutoka ASEC Mimosas ya kwao Ivory Coast.

Aubin Kramo Kouamé Simba SC
Simba pia inaiwinda saini ya winga, Aubin Kramo Kouamé mwenye umri wa miaka 27 kutoka ASES Mimosas ya Kwao Ivory Coast pia.

Leandre Willy Essomba Onana Simba SC
Klabu ya Simba imetajwa kuwa kwenye mazungumzo na Winga Leandre Willy Essomba Onana mwenye umri wa miaka 23 kutoka Rayon Sports ya kwao Rwanda.
Onana ndiye Kinara wa Ufungaji katika Ligi Kuu ya Rwanda (Rwanda Premier League) akiwa na magoli 15 na assist 10.

Hassan Saleh Dilunga Simba SC
Klabu ya Simba imekamilisha usajili wa aliyekuwa kiungo wao, Hassan Saleh Dilunga kwa mkataba wa mwaka mmoja wenye kipengele cha kuongezewa mwingine.
Klabu ya Young Africans SC, ipo kwenye Mazungumzo ya kumsajili Mshambuliaji Khanyisa Mayo mwenye umri wa miaka 24 kutoka Cape Town City ya Afrika Kusini.
Mayo ndiye Kinara wa Ufungaji Ligi Kuu ya Afrika Kusini (South African Premier Division), akifunga mabao 12 sawa na Peter Shalulile wa Mamelodi Sundowns.
Young Africans pia inahusishwa na Mshambuliaji wa Marumo Gallants, Ranga Chivaviro mwenye umri wa miaka 30.
Chivaviro ndiye Kinara wa Ufungaji kwenye Kombe la Shirikisho Afrika, akiwa na magoli matano (5) sawa na Fiston Mayele wa Yanga SC, huku kwenye Ligi Kuu ya Afrika Kusini (South African Premier Division), akiwa na magoli 9 kwenye michezo 17.
Klabu ya Simba SC inamnyatia kiungo mkabaji mahiri, Gatoch Panom Yiech raia wa Ethiopia mwenye umri wa miaka 28 KutokaSt. George SC ya kwao Ethiopia.
Mkataba wa Yiech Panom Gatoch na St. George SC unatajiwa kufikia tamati June 30, 2023.

Fred Felix Minziro Mbeya City FC
Kocha, Fred Felix Minziro huenda akajiunga na Mbeya City kama Kocha wao Mkuu kuanzia msimu ujao wa 2023/2024 akitokea Geita Gold FC.

Yassin Mustapha Singida Big Stars FC
Klabu ya Singida Big Stars FC imepanga kuachana na wachezaji watatu ambao ni beki wa kati Pascal Wawa, Yassin Mustapha na Mshambuliaji Hamis Tambwe mwishoni mwa msimu huu wa 2022/2023.

Paul Nonga Mbeya City FC
Mshambuliaji wa klabu ya Mbeya City, Paul Nonga anatarajiwa kuacha kucheza rasmi soka la ushindani mwishoni mwa msimu huu wa 2022/2023.
Baada ya kustafu mpira wa miguu mchezaji huyo atakabidhiwa timu ya vijana ya Mbeya City kama kocha Mkuu.

Gustapha Saimon Coastal Union FC
Vilabu vya Dodoma Jiji, Kagera Sugar na Mtibwa Sugar vimeonesha nia ya kutaka saini ya nyota Gustapha Saimon kutoka Coastal Union FC.

Gadiel Michael Singida Big Stars FC
Beki wa Simba, Gadiel Michael na Mshambuliaji Habibu Kyombo wapo Katika hatua za mwisho kutua Singida Big Stars ya Mkoani Singida.
Young Africans pia ina mpango wa kuachana na winga wao Tuisila Rossien Kisinda mwenye umri wa miaka 23 kutoka DR Congo mwishoni mwa msimu huu.
Wachezaji wengine ambao Young Africans ina mpango wa kuachana nao kuelekea msimu ujao wa 2023/2024 ni Benard Morrison mwenye umri wa miaka 29, David Bryson, Crysin Ngushi, Dickson Ambundo na golikipa Eric Johora.
Beki wa Kimataifa wa Kenya, Joash Onyango mwenye umri wa miaka 30 ametajwa kuwasilisha barua ya maombi ya kuomba kuondoka katika klabu hiyo aliyoitumikia takribani miaka mitatu.
KLABU ya Singida Big Stars inaidaiwa kukamilisha usajili wa beki wa kulia Nicolas Wadada kutoka Ihefu SC.
Huo utakuwa usajili wa pili wa Singida Big Stars baada ya kukamilisha usajili wa beki Yahya Mbegu kutoka Ihefu SC, ambaye alikuwa kwenye rada za Simba SC.
Uongozi wa klabu ya Young Africans upo kwenye mazungumzo ya kumuongezea mkataba mpya wa miaka mitatu (3) golikipa wao Metacha Mnata, baada ya mkataba wa mkopo wa miezi 6 kutoka Singida Big Stars kuisha mwishoni mwa msimu huu.
Wachezaji wengine ambao Young Africans inajadiliana nao kwaajili ya kuongeza mkataba mpya ni Jesus Moloko na Denis Nkane.
Beki wa kati wa Klabu ya Young Africans, Ibrahim Abdallah Hamad amefikia makubaliano ya kuongeza mkataba wa kuendelea kuwatumikia wananchi kwa miaka mitatu ijayo.
Klabu ya Simba SC ipo kwenye mazungumzo na kinda wa Geita Gold FC, Edmund John mwenye umri wa miaka 20.
Imeelezwa kuwa Klabu ya Simba ina mpango wa kuachana na Wachezaji wake 11 kuelekea msimu mpya wa 2023/2024.
Wachezaji hao waliotajwa ni Nelson Okwa na Patrick Victor Akpan wote kutoka Nigeria, Augustine Okrah kutoka Ghana, na Mohamed Ouattara kutoka Ivory Coast
Wengine ni Hamed Ismael Sawadogo kutoka Burkina Faso, Peter Banda Kutoka Malawi, Jimmyson Mwanuke, Nassoro Kapama, Beno David Kakolanya, Jonas Gerald Mkude na Gadiel Michael Kamagi wote Watanzania.
Klabu ya Simba SC imetajwa kukamilisha Usajili wa beki wa kushoto Yahya Mbegu kutoka Ihefu SC ya Mbeya ili kuziba nafasi ya Gadiel Michael anayeachwa.
Klabu ya Simba SC ipo kwenye mpango wa kuwasajili viungo, Sospeter Bajana, anayemaliza mkataba wake na Azam msimu huu pamoja na Brno Gomez kutoka Singida Big Stars FC.
Wengine walio kwenye mpango wa Simba SC ni kipa Fabien Mutombola na Mshambuliaji Martin Kizza wote kutoka Vipers ya Uganda.

Benard Morrison Singida Big Stars FC
Klabu ya Singida Big Stars imetajwa kuwa katika hatua za mwisho kukamilisha Usajili wa kipa wa Simba SC, Beno Kakolanya, wengine ambao Singida inatajwa kuwinda saini zao ni Benard Morrison kutoka Yanga SC.

Juma Mgunda Simba Sc
Klabu ya Coastal Union ya Tanga ipo kwenye mazungumzo na kocha wao wa zamani, Juma Mgunda ya ili awe kocha wao ajaye kwa msimu ujao wa 2023/2024.
Golikipa nambari mbili wa Simba SC, Beno David Kakolanya amekataa ofa ya kwanza kutoka kwa timu ya kutaka kumuongeza mkataba mpya wa kuendelea kuitumikia klabu hiyo yenye makazi yake Mtaa wa Msimbazi Jijini Dar es salaam.

Beno David Kakolanya Sinba SC
Inaelezwa kiwa kipa huyo amepewa ofa ya mshahara wa milioni tano (5m) kwa mwezi pamoja na ada ya usajili milioni 60.
Kakolanya amekataa ofa hiyo na kutoa sababu kuwa anataka kwenda sehemu nyingine ili awe anapata nafasi ya kucheza.

Yassin Mstafa Singida Big Stars FC
klabu ya Singida Big Stars huenda ikaachana na beki wake wa pembeni, Yassin Mstafa mwishoni mwa msimu huu, kutokana na ufinyu wa nafasi ndani ya Kikosi hicho cha walima Alizeti.

Yahaya Mbegu Ihefu SC
Kuna uwezekano mkubwa wa beki wa pembeni wa klabu ya Ihefu SC, Yahaya Mbegu kujiunga na Singida BS msimu ujao wa 2003/2024.

Habibu Kyombo Simba Sc
Singida Big Stars pia ipo kwenye mazungumzo ya kumrudisha aliyekuwa Mshambuliaji wake, Habibu Kyombo endapo Klabu ya Simba itaamua kumuachia mwishoni mwa msimu huu.

Fred Felix Minziro Geita Gold FC
Klabu ya Geita Gold ya mkoani Geita huenda ikaachana na Kocha wake Mkuu, Fred Felix Minziro kabla ya msimu huu kumalizika au mwishoni mwa msimu huu.
Taarifa kutoka ndani ya viunga vya Geita Gold zinasema kuwa Uongozi wa klabu hiyo unafikilia kuachana na Minziro kwa sababu ya kutokuwa na maelewano na wasaidizi wake wa benchi la ufundi.

Thierry Manzi Simba SC
Klabu ya Simba imetajwa kumwania beki wa kati na Nahodha Msaidizi wa timu ya taifa ya Rwanda, Thierry Manzi mwenye umri wa miaka 26 kutoka AS Kigali ya kwao Rwanda.

Eric Benjamin Kabwe Simba SC
Simba pia ipo kwenye Mazungumzo na Mshambuliaji Eric Benjamin Kabwe mwenye umri wa miaka 22 kutoka AS Vita Club ya kwao DR Congo.

Ibrahim Abraham Singida Big Stars FC
Klabu ya Singida Big Stars ipo kwenye hatua za mwisho kukamilisha usajili beki wa kulia wa Tanzania Prisons ya Mbeya, Ibrahim Abraham.

Arakaza MacArthur Geita Gold FC
Klabu ya Geita Gold ipo kwenye Mazungumzo ya kumuongezea Mkataba golikipa wao, Arakaza MacArthur raia wa Burundi baada ya kuridhishwa na kiwango chake.
Klabu ya Kitayosce FC ya mkoani Tabora, iliyopanda Ligi Kuu ipo kwenye hatua za mwishoni kukamilisha Usajili wa wachezaji wanne (4) kwaajili ya kusuka kikosi upya kuelekea msimu ujao wa 2023/2024.

Yacouba Sogne & Heritier Makambo Kitayosce FC
Wachezaji wanaotajwa kuwaniwa na Kitayosce ni Washambuliaji Yacouba Sogne kutoka Ihefu SC, pamoja na Heritier Makambo ambaye hana timu, golikipa Wilbol Maseke Changarawe kutoka Azam FC na Beki Steven Duah kutoka Kagera Sugar.

Crescentius Magori vs Mo Dewji’Mo’ Simba SC
Inaelezwa kuwa Mdhamini na Rais wa Heshima wa Klabu ya Simba SC, Mohamed Dewji ‘Mo’ amemrejesha kwenye Bodi ya Simba aliyekuwa CEO wa zamani wa timu hiyo Crescentius Magori kwaajili ya kuongeza nguvu ya utendaji kazi ndani ya Bodi hiyo kuanzia Msimu ujao 2023/2024.

Jonas Mkude, Gadiel Michael & Augustine Okrah Singida Big Stars FC
Wachezaji wanaoondoka Simba SC msimu ujao wa 2023/2024 ni pamoja na Ismail Sawadogo, Augustine Okrah, Gadiel Michael anaenda Singida Big Stars FC, Habibu Kiyombo anaenda Singida Big Stars FC, Jonas Mkude anaenda Singida Big Stars pia, mwingine ni Mohammed Outtara, huku Joash Onyango akiwa 50%/50%.

Mahamoud Mroyvil _ Emery Nimubona Coastal Union FC
Klabu ya Coastal Union FC ya Tanga imeachana na golikipa wake Mahamoud Mroyvil pamoja na beki wake wa kulia Emery Nimubona raia wa Burundi.
TETESI za Usajili NBC Premier League 2023/2024, Tetesi za Usajili Simba 2023,Tetesi za Usajili Tanzania,Usajili NBC 2022/2023, Tetesi za Usajili Yanga 2023,Usajili wa Simba Dirisha Kubwa 2023,Usajili wa Yanga Dirisha Kubwa 2023, Tetesi za Usajili Simba dirisha Kubwa 2023,Tetesi za Usajili Yanga dirisha Kubwa 2023,Tetesi za Usajili Young Africans 2023,Tetesi za Usajili Simba SC 2023.
PIA UNAWEZA KUSOMA👇
- FAHAMU kuhusu Azam Pesa pamoja na Makato yake
- Ada mpya za M-Pesa 2023/2024 | Makato mapya ya M-Pesa
- DOWNLOAD | NYIMBO ZA TENZI ZA ROHONI SWAHILI MIX
- Ada za M-Pesa Songesha 2022/2023
- FAHAMU Jinsi ya Kufungua Akaunti ya M-Koba Vodacom
- MFUMO wa maombi ya Kitambulisho cha Taifa (NIDA) Online
- JINSI ya kupata mikopo ya vijana na wanawake
- Namna ya Kujisajili na Premier Bet Ushinde Mamilioni
- RATIBA kamili NBC Premier League msimu wa 2022/2023
- DOWNLOAD NIDA number | Kitambulisho cha Taifa
- MSIMAMO Ligi Kuu Tanzania Bara 2022/2023
- WAFUNGAJI Wanaoongoza kwa Ufungaji Ligi Kuu
Nijuze TV ni App ambayo ukiwa nayo utaweza kutazama mechi za Ligi Kuu Tz Bara (NBC PREMIER LEAGUE) EPL, WORLD CUP, EPL, LALIGA, SERIA, LIGUE 1, BUNDESLIGA na Ligi nyingine nyingi.

Download App ya Nijuze Habari Playstore tukutumie Habari zote kwenye Simu yako BILA MALIPO BOFYA HAPA.

Tags: Dondoo na tetesi za Usajili Ligi Kuu Tanzania Bara 2023/2024, Tetesi za Usajili NBC Premier League, TETESI za Usajili NBC Premier League 2023/2024, Tetesi za Usajili NBC Premier League Tanzania 2023/2024, tetesi za Usajili Simba 2023, Tetesi za Usajili Simba dirisha Kubwa 2023, tetesi za usajili Simba sc 2023, Tetesi za Usajili Tanzania, Tetesi za Usajili Tanzania 2023/2024 NBC Premier League., Tetesi za Usajili Yanga 2023, Tetesi za Usajili Yanga dirisha Kubwa 2023, Tetesi za Usajili Young Africans 2023, Usajili NBC 2022/2023, Usajili wa Simba Dirisha Kubwa 2023, Usajili wa Yanga Dirisha Kubwa 2023