ZIFAHAMU aina za Madaraja ya Leseni za Udereva Tanzania

AJIRA MPYA ZA WIKI HII BONYEZA HAPA
AUDIOS MPYA ZA WIKI BONYEZA HAPA
VIDEOS MPYA ZA WIKI HII BONYEZA HAPA


ZIFAHAMU aina za Madaraja ya Leseni za Udereva Tanzania

ZIFAHAMU aina za Madaraja ya Leseni za Udereva Tanzania
A-Pikipiki zenye Ukubwa wa zaidi ya 125CC au uzito wa 230Kg ikiwa na kigari pembeni au isiyokuwa na kigari.
A1 – Pikipiki zenye Ukubwa chini ya 125CC au uzito 230kg na isiyokuwa na kigari pembeni.
A2 – Kuendesha pikipiki za magurudumu matatu au manne.
A3 – Mitambo ya kukatia majani au pikipiki zisizozidi 50CC.
B – Magari aina zote (Binafsi) ISIPOKUWA Magari ya Biashara, Magari Makubwa ya Mizigo na Pikipiki.
C – Magari ya kubeba abiria kuanzia 30 na kuendelea.
C1 – Magari ya kubeba abiria 15 hadi 29.
C2 – Magari ya kubeba abiria 4 hadi 14.
C3 – Magari ya kati ya abiria 4 hadi 14.
D-Magari aina zote ISIPOKUWA Magari ya Abiria, Magari Makubwa ya Mizigo na Pikipiki.
E-Magari aina zote ISIPOKUWA Magari ya Abiria na Pikipiki.
F – Mitambo kama Graders, Folklift n.k
G – Mitambo ya Mashambani na Migodini kama Tractors n.k
H – Leseni ya kujifunzia kuendesha Gari.
NB: Unapokuwa na Daraja D huna haja ya kuwa na daraja B kwa kuwa daraja D hujumuisha magari yaliyo katika daraja B ila ukiwa na daraja B huwezi endesha daraja D.
Pia ukiwa na daraja A si kigezo cha kuendesha madaraja yote ya A, utaendesha Madaraja yote ya A isipokuwa A2 ambayo ni Pikipiki za Magurudumu Matatu/Manne.
Kuomba Leseni ya Udereva kwa mara ya kwanza ni lazima uwe umehudhuria mafunzo katika Chuo chochote kinachofahamika na kupewa cheti.
Pia uwe na umri zaidi ya miaka 18 kwaajili ya Gari na umri wa miaka 16 na kuendelea kwaajili ya pikipiki.
Uwe na Leseni ya kujifunzia/ya muda ya Udereva.
Uwe umelipa Ada ya kufanyiwa majaribio – GRR.
Uwe na Cheti cha kupimwa macho, uwe umepeleka maombi kwenye ofisi ya Polisi wa Usalama Barabarani kwaajili ya kufanyiwa majaribio.
Uende kwenye Ofisi ya Polisi wa Usalama Barabarani ukiwa na Gari kwaajili ya kufanyia majaribio.
Baada ya mwombaji kufanyiwa majaribio anaweza kuruhusiwa kuendesha pikipiki na magari madogo.
Kubadilisha leseni ya udereva (Daraja A B C D E F na G)
- Mwombaji ataenda kwenye ofisi ya polisi wa usalama barabarani akiwa na leseni yake ya zamani ya udereva
- lazima awe na cheti cha umahiri
- mwombaji awe na umri zaidi ya miaka 18 kwa magari na miaka 16 kwa pikipiki
KUBADILI ILI KUPATA DARAJA ”C”
- Mwombaji ataenda katika ofisi ya polisi wa usalama barabarani akiwa na leseni yake ya zamani ya udereva
- Awe na cheti cha umahiri
- Mwombaji awe na umri zaidi ya miaka 18 kwa magari na miaka 16 kwa pikipiki
- Cheti cha Gari la Kubeba Abiria (PCV) kutoka Chuo cha Taifa cha Usafirishaji au VETA
- Mwombaji anatakiwa kubainisha aina ya gari analokusudia kuendesha
- Mwombaji atapewa daraja la leseni kulingana na mafanikio yake.
Ni viwango gani vinatumika?
Ada za leseni | Shilingi 40,000/= itakayolipwa kila baada ya miaka 3 |
Ada ya jaribio la kuendesha | Shilingi 3,000/= |
Ada za leseni ya muda | Shilingi 10,000/= itakayolipwa kila baada ya miezi 3 |
- RATIBA kamili ya hatua ya 16 Bora Azam Sports Federation Cup 2023
- RATIBA kamili NBC Premier League msimu wa 2022/2023
- DOWNLOAD NIDA number | Kitambulisho cha Taifa
- MSIMAMO Ligi Kuu Tanzania Bara 2022/2023
- WAFUNGAJI Wanaoongoza kwa Ufungaji Ligi Kuu
- RATIBA ya Yanga CAF Confederation Cup 2022/2023 hatua ya Makundi
- RATIBA ya Simba CAF Champions League hatua ya Makundi
Nijuze TV ni App ambayo ukiwa nayo utaweza kutazama mechi za Ligi Kuu Tz Bara (NBC PREMIER LEAGUE) EPL, WORLD CUP, EPL, LALIGA, SERIA, LIGUE 1, BUNDESLIGA na Ligi nyingine nyingi.
DONWLOAD NIJUZE TV HAPA SISI kwetu Michezo ndiyo Furaha YETU.
Download App ya Nijuze Habari Playstore tukutumie Habari zote kwenye Simu yako BILA MALIPO BOFYA HAPA.
Download App ya Nijuze TV Utazame mechi zote kwenye Simu yako BOFYA HAPA
Tags: Aina ya Madaraja ya Leseni za Udereva Tanzania, Maana ya Picha za Leseni ya Udereva Tanzania, Madaraja ya Leseni za Udereva Tanzania, ZIFAHAMU aina za Madaraja ya Leseni za Udereva Tanzania